Van Persie Amtaka Raheem Sterling Kuipambania Feyenoord

Kocha wa Feyenoord, Robin van Persie, ameweka wazi kuwa anatarajia makubwa zaidi kutoka kwa winga Raheem Sterling, ambaye bado hajafikia kiwango kilichotarajiwa tangu ajiunge na klabu hiyo. Nyota huyo wa England ameendelea kuwa gumzo kufuatia kiwango chake kisichoridhisha katika mechi za hivi karibuni.

Van Persie Amtaka Raheem Sterling Kuipambania Feyenoord

Licha ya kiwango kibovu, Van Persie hajamkatia tamaa mchezaji huyo mwenye uzoefu mkubwa. Ameeleza kuwa anafanya kazi kwa karibu sana na Sterling ili kuhakikisha anarudi kwenye ubora wake, akisisitiza kuwa mchezaji huyo anaelewa wazi nini kinahitajika kuboreshwa.

Baada ya mchezo wa De Klassieker dhidi ya Ajax uliomalizika 1-1, Van Persie alifanya mazungumzo ya kina na Sterling, akimweleza moja kwa moja matarajio yake. Kocha huyo amesema anampa maelekezo ya wazi na makali, akiamini kuwa wachezaji wakubwa wanapaswa kuhimili presha hiyo.

Van Persie Amtaka Raheem Sterling Kuipambania Feyenoord

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Hadi sasa, Sterling amecheza dakika 256 tu katika mechi tano rasmi, huku mchango wake mkubwa ukiwa asisti moja muhimu dhidi ya Excelsior. Hii inaonyesha bado hajapata muendelezo wa kiwango unaohitajika kuisaidia timu.

Van Persie Amtaka Raheem Sterling Kuipambania Feyenoord

Kwa mechi sita zilizobaki msimu huu, presha iko juu kwa Sterling kujidhihirisha na kusaidia Feyenoord kufikia lengo lao la kufuzu Ligi ya Mabingwa. Huu ndio wakati wake wa kuthibitisha kuwa bado ana uwezo wa kuwa mchezaji wa kiwango cha juu.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.