Bara la Afrika limekuwa na washambuliaji wafungaji mabao mahiri sana tangu enzi na enzi katika ligi mbalimbali duniani kote. Hata hivyo, kuna waliotisha zaidi ya wengine wote. Angalia hapa chini kuwafahamu:
Inaendelea…
George Weah
Rais wa sasa wa taifa la Liberia alikuwa anatisha sana katika soka la ulimwenguni enzi zake za ujana kabla hajashinda uchaguzi wa taifa lake mwaka 2017. Yeye ni mchezaji soka pekee wa Afrika ambaye ameshinda tuzo zote za FIFA World Player of the Year na ile tuzo nzuri sana na kubwa duniani, Ballon d’Or.
Alibarikiwa sana kuwa na kipaji na ujuzi wa soka na uwezo mkubwa sana wa kuona goli lilipo, kwa sasa ana umri wa miaka 53 na ameshinda medali nyingi sana akiwa na klabu mbalimbali na hata akiwa yeye binafsi.
Ukiachilia mbali suala la yeye kuwa ameshinda tuzo ya African Player of the Year mara tatu, Rais huyo wa Liberia alikuwa ndiye mfungaji bora kwa msimu wa 1994/1995 wa michuano ya Champions League.
Alishinda kombe la FA Cup akiwa na klabu ya soka ya Chelsea na lile la Ligue 1 akiwa na klabu ya soka ya Olympique Marseille.
Inasikitisha sana kuwa huyu Weah hakushinda lolote akiwa na taifa lake hilo. Ila hata hivyo bado anabakia kuwa ndiye moja ya washambuliaji wakubwa sana na walio bora kutoka Afrika.
Roger Milla
Roger Milla aliiwakilisha nchi yake kwenye mashindano ya 1990 World Cup kule nchini Italia na iliweka historia kubwa ambayo inadumu mpaka leo hii. Mcameroon huyo alikuwa na umri wa miaka 38 wakati alipoisaidia timu ya The Indomitable Lions kufunga mabao manne na kuweka historia ya kuwa ndiye mchezaji wa kwanza wa Afrika kufika hatua ya robo fainali.
Miaka minne mbele akiwa USA akafanikiwa kuwa ndiye anayeongoza katika ufungaji magoli akiwa na umri mkubwa zaidi ya wengine kwa wakati huo.
Mafanikio haya, hata hivyo, yalikuja mwishoni mwa soka lake la kimataifa. Kwa ujumla tunaweza sema kuwa alishinda mataji ya AFCON mara mbili, AFCON Golden Boot mara mbili na vile vile akawa ndiye Player of the Tournament mwaka 1986.
Tusisahau kuwa mkongwe huyu alitunukiwa kuwa ndiye African Player of the Year mara mbili, na pia CAF ikamtaja mara mbili kuwa ndiye Africa’s Player of the Century.
ITAENDELEA…


Salma
Hii ni mpya kwangu nasubili muendelezo
Antony Luseno
George weah ndo anafahamika kama king wa football afrika lakin watu kama Drogba ni zaidi mno
Ester jackson
Asante kwa taarifa nzuri sikujua kama kunawatu walikuwa na kipaji kikubwa na kufikia kuwa viongozi wanchi
Neema juma
Roger Milla ajitahidii azidi kutuletea historia nzuri afrika ki mchezo
Samiah
Nihistoria nzr sanaa afrika kimchezo
Theckla
Makala nzuri nasubiri mwendelezo
Elika
Africa ni bara lenye vipaji sana hasa vya mpira
Agness
Asantee meridani kwa makala nzuri
Hope mwaikuka
Bora umenijuza
Adelta
George weah Ni fundi mzuri wa mpira
Neema hassan
Kumbukumbu nzuri kwa vizazi vijavyo..
felister
habari nzuri kwa wapenzi wa soka
Khadija
Tupo pamoja meridian kwa makala zenu#meridianbettz
Rehema
Bonge la makala aiseee
Isaya massawe
Pongezi kwao walitisha sana
#meridianbettz
Sadick
Kwangu mimi George Weah anasitahili kudo. Mafanikio ktk ngazi ya Timu ya Taifa yanategemea mambo mengi ambayo mengi yalikuwa nje ya uwezo wake #meridianbettz
Warda
Milla namkubali kitambo sana#Meridianbettz
Aziza mushi
Makala nzuri Sana nasubiri mwendelezo.
Ester mmakasa
Afrika ni bara lenye vipaji vingi vya kila aina sio kwenye soka tuu.
Tahiya
Ni makala nzur kwakwer najivunia kuwa mwafrika hakika kuna vipaji vingi sana hasa mpira
Shafii
Makala nzur
David Pere
George alitisha na Ndio mchezaji pekee duniani aliyeweka record ya kuchukua tuzo tatu kubwa kwa mwaka mmoja
winfrida
Afrika ni kituo cha wachezaji walio bora duniani isipokua shida ni ule uafrika wao
Frank Patrick
Seeing is Believing….Drogba was the best to Me
mwakalosi
kwa leo Roger milla japo George weah anamafanikia zaid
Amani
Roger Milla alikuwa mchezaji Babu kubwa na atari sana
Ernest
Africa tunavipaji sana sema msingi mzuri hatuna na bado wanatubania kwenye tuzo.
lombo
Rogar miller namkubali sanaa
Lydia Emmanuel Magoti
Rogar Milla alikuwa mchezaji mzuri Sana jembe
Gabriel
Wakal sana hao watu
Genia Sikaluzwe
Makala nzuri Sana hii na subili muendelezo
Caroline
Africa tuna vipaji
Theonestina
Asanteni meridianbet kwa taarifa
Dorophina
Asante meridian kwa taarifa maana sikuwahi kuisikia
Kenani
Safi kabisa
Latifa juma mohamed
Makala nzuri ,Africa tuna vipaji vya pekee
Asia Abdy
Tunajivunia wa Africa
Emmy cleopa
Habar njema
Rehema Dickson
Bara la africa mungu karijaalia sana vipaji na watu wa kujituma kutumia vipaji vyao kama ajira hongerin sana sana
isha
Afrika mungu ametujalia vipaji na tunajua kivitumia
Hamidu
George weah. Nakubali Sana
Mwanahamisi
Hao watu balaa
Povel
Weah ni mtu mwenye bahati na mafanikio ni mfano wa kuigwa
Magdalena
Roger Milla namkubali Sana Ila naisubiria mwendelezo
Mariam mtandama
Habari mjema