Watatu Wakutwa na Corona FC Koln

Watu watatu katika klabu ya FC Koln wamekutwa na maambukizi ya Corona, klabu hiyo imethibitisha japo wamesema mazoezi yataendelea kama ilivyopangwa. Koln ipo imebakiwa na mechi tisa na wapo nafasi ya kumi.

Bundesliga inatarajia kuwa Ligi ya kwanza Ulaya kurejea uwanjani.

Tarehe rasmi iliyotajwa ni tarehe 9 Mei lakini serikali imechelewa kufanya maamuzi ya kurejea hivyo kufanya tarehe kusogea hadi Mei 16 au 23.

Wale waliokutwa na virusi hawakuwa na dalili yoyote lakini watakaa karantini siki 15 imesema klabu.

“Wachezaji wote, makocha na watumishi wengine walipima Alhamis Covid-19,”

“FC Koln hawatataja majina kwa kuheshimu usiri wa walioathirika. Mazoezi yataendelea kama ilivyopangwa kwa kuzingatia taratibu zote za kuzuia maambukizi ambazo zimewekwa tangu April 6 kwenye mazoezi ya vikundi.

“Tumechukua hatua za kupima kikundi hicho tena, kama ushauri wa wataalamu wa afya ‘Taskforce Sports Medicine/Special Game Operation’ kutoka DFL.”

Alhamis, Chancellor Angela Merkel alisema maamuzi yoyote kuhusu lini shughuli za michezo zitarejea yatafanyika Jumatano Mei 6.

Chancellor Angela Merkel

“Ni muhimu kutulia na kuheshimu taratibu za wataalamu wa afya,” alisema Merkel.

21 Komentara

    Duh ukisia supu imetiwa nazi ndio hii!

    Jibu

    Duuh unaweza onachongo ukazani kengeza hapo

    Jibu

    Ni muhimu kujua afya yako kwanza alafu mengine yanafuata, wapimwe ili wakianza wameanza

    Jibu

    Hii Corona jamanii

    Jibu

    Mungu awape afya njema wapone haraka warejee kiwieanjani

    Jibu

    Daah majanga.

    Jibu

    Bora waanze tu lile joto la mazoez Corona atakimbia mwenyew

    Jibu

    Sasa itakuaje jamani, Corona hiiii

    Jibu

    Daaah mungu awaponye jmn

    Jibu

    Duh !mungu awafanyie wepesi wapone na waweze kurejea uwanjan wakiwa na afya njema

    Jibu

    Mungu awafanyie wepesi wapone kwa halaka

    Jibu

    Mungu awasaidie wapone haraka warejee uwanjani

    Jibu

    Mungu awasaidie

    Jibu

    Pole ya wachezaji waliokutwa na maambukizi

    Jibu

    Mwenyezi mungu awanusuru awape afya njema

    Jibu

    🙏

    Jibu

    Mambo yanazid kuwa magumu uko

    Jibu

    Mungu awasaidie wapone

    Jibu

    Mungu atulinde Mana hatuna ujanja

    Jibu

    Tuombeane kwa kweli

    Jibu

    Duuh poleni sana

    Jibu

Acha ujumbe