Willian Asaini Kandarasi ya Mwaka Mmoja Fulham

Mshambuliaji wa kimataifa wa Brazili na klabu ya Corinthians leo amesaini kandarasi ya mwaka mmoja na klabu ya Fulham baada ya kuvunja mkataba wake na klabu ya Corinthians.

Wilian mwenye miaka 34 ameichezea timu yake ya taifa michezo 70. Pia amekuwa akifanya mazoezi kwenye viunga vya Motspur Park kwa takribani wiki tatu sasa anatarijiwa kuwa chini ya kocha Marco Silva ambapo natarajiwa kwenda kusaidiana na Harry Wilson na Manor Soloman ambao kwa sasa ni majeruhi.

Willian kwnenye wakati waki wakiwa kama mchezaji wa chelsea amefanikiwa kushinda kila kombe nchini Uingereza ambalo klabu hiyo imeshiriki kwenye viunga vya Stamford Bridge, Willian aliondoka kwenye klabu hiyo ya nyumbani kwao mwezi mmoja uliopita na sasa  yupo nchini uingereza kukamilisha uhamisho huo.

Willian aliuwambia mtandao wa Fulham: “Nina furaha kuwa hapa, ninafuaha kurudi kwenye ligi kuu ya Uingereza. Fulham ni klabu ya Pekee, klabu ambayo inataka kujiboresha, hicho ndicho inachotaka kupigania ili kupata kitu kikubwa, hivyo nio hapa kusaidia, ninashauku ya kuweza kuanza.”

 

Acha ujumbe