Baada ya kufunga usajili wao kwa kishindo kwa kumshusha mshambuliaji hatari wa timu ya Taifa ya Burundi, Fiston Abdoul Razak. Uongozi wa klabu ya Yanga umesema hesabu zote zimekamilika na kilichobaki ni vita ya kuhakikisha wanatwaa ubingwa msimu huu.

Fiston aliyetua rasmi siku ya Ijumaa iliyopita akitokea nchini Burundi, na kupelekwa moja kwa moja kujiunga na kambi ya timu hiyo anakamilisha idadi ya wachezaji watatu waliosajiliwa na Yanga katika kipindi cha usajili wa dirisha dogo.
Wachezaji wengine wa Yanga waliosajiliwa ni; Dickson Job na Saidi Ntibazonkiza, huku Yanga pia ikiongeza nguvu kwenye benchi lake la ufundi kwa kumwajiri kocha msaidizi Nizar Khalfan na kocha wa viungo raia wa Ghana Edem Mortotsi.

Akizungumzia mipango yao katika mzunguko wa pili wa ligi Mkurugenzi wa uwekezaji wa GSM na mjumbe wa kamati ya usajili Injinia, Hersi Said amesema: “Tumekamilisha kwa kiasi kikubwa mipango tuliyokuwa nayo kabla ya kuanza kwa msimu huu, ambapo shabaha yetu kubwa ilikuwa ipo katika maeneo matatu ya utawala bora, idara ya ufundi iliyo thabiti na wachezaji wa kiwango cha juu.
“Kazi hiyo tumeikamilisha kupitia usajili bora wa wachezaji na kuajiri makocha wenye viwango na wakati huu tumebaki na lengo moja tu la kuhakikisha tunaibuka mabingwa msimu huu.
Neptune’s Richies ni mchezo Unaokupa pesa chap chap huku ukiwa unaburudika kupitia Kasino ya Mtandaoni ndani ya Meridianbet.



Janeflora malisa
Asnt kwa taarif meridianbet
Issa
Msimu huu mtatujua
Magdalena
Kila la kheri kwao
Rahma
Saw tunasubili tuone
Adelta
Sawa ngoja tusubiri yatakayo jiri
Caroline
Yanga mbele daima
Dorophina
Daima mbele nyuma mwiko
Venerose
Mmh tunasubir tuone
Sarah
Kila lakheri yanga
Hopemwaikuka
Hongeren
Amiri Kayera
Daima mbele
Sania
Utopolo msituletee maneno tunataka vitendo
Lydia Emmanuel Magoti
Ngoja tuone
warda
Hawapati hata kwa nini