Klabu ya Yanga SC imekamilisha usajili wa Golikipa na kapteni wa Mtibwa Sugar Aboutwalib Hamidu Mshery kwa mkataba wa miaka miwili na nusu.

Msheri ambaye ni kipa wa timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 23 amejiunga na Yanga SC kuziba nafasi iliyoachwa na Djigui Diarra aliyejiunga na timu ya taifa kwenye mashinda no ya AFCON.
“Tayari tumemalizana na Msheri ambaye usajili wake umependekezwa na kocha Nesreddine Nabi, akiamini atakuja kuongeza changamoto kwa Djigui Diarra na Erick Johora, “alisema Afisa habari wa Yanga SC, Hassan Bumbuli.
Msheri atavalia jezi nambari 28 katika kipindi cha miaka miwili na nusu atakayokuwepo jangwani huku akitarajiwa kuwepo katika mchezo wa tarehe 31 dhidi ya Dodoma jiji.
Unaanzaje siku yako katika msimu huu wa sikukuu, mchongo upo meridianbet kasino. Sloti pendwa ya Sahara Richies inaweza kukufanya ukawa milionea katika kufunga mwaka huu, Jiunge na ufurahie kasino maridhawa kutoka nyumba ya mabingwa.

CHEZA HAPA

