Ili kushinda vita ni lazima ujue muda gani upambane, muda gani ujifiche na muda gani ukimbie, bila shaka unamkumbuka Zidane kwenye ubora wake, alikua ni Goliath wa soka, lakini mtoto mdogo tu Marco Materrazi alitumia akili ndogo kumshinda

Katikati ya ubora na ufundi mkubwa na kuibeba Ufaransa mgongoni mwake, ila Zidane akaja kuwa adui mkubwa na kusemwa sana na Wafaransa, Zizzou alimuuliza Materrazi “Unahitaji jezi yangu?” ila Materrazi alimjibu “Namtaka Dada yako”, hapo Zizzou aligeuka kuwa Mwarabu halisi, akala umeme fainali world cup 2006 pale German
Yupo wapi yule Daudi aliemwangusha Binadamu aliesimama kwenye ukumbi mmoja pale Basel Uswizi, 2003 akibeba tuzo ya mchezaji bora wa dunia, alikua ni General wa soka na Maestro uzawa wa Algeria, haikuwa tuzo yake ya mara ya kwanza au ya pili bali ni ya tatu
Pengine labda Daudi hakujua kuwa alimuangusha Goliath, aliefanya makubwa kwenye tuzo kabla ya ujio wa Ronaldo na Messi, labda amesahau kuwa baada ya kichwa cha Angelos Charisteas kilichowatoa France robo fainali ya Euro 2004, Zizzou alitangaza kustaafu

Lakini tangazo lake lilikataliwa na Wafaransa wote, Kocha Raymond Domenech na wanasiasa nguli kama Nicolaus Sarkozy, kila mtu alitaka arejee uwanjani, akakubali kuvaa upya viatu vyake, kuvaa upya kitambaa chake na jezi yake namba 10 ya Les Blues, kwa ajili ya kombe la dunia 2006
Alirejea wakati ambao timu ilimuhitaji zaidi, wakahitaji pass zake, swashbuckling, tantalizing football na Panenka zake, aliibeba timu mgongoni mwake mpaka zile fainali pale Ujeruman, hakuna aliejua kuwa mwisho wake utakua mbaya zaidi ya ule wa 2004
Nakumbuka pia Goliath alitangaza kustaafu soka la klabu Mei 7 pale Bernabeu, uwanja ulijaa nembo ya ‘Zidane 5’, alipiga goli lake la mwisho kwenye ile sare ya 3-3 dhidi ya Villareal mbele ya Alfredo di Stefano, ilikua cross ya Beckham, baadae alirejea kuwaaga na machozi yakimtoka sana


Salma
Hii ni mpya kwangu mko vizuri kwa habari
Ester jackson
Kwake anaona sawa mana kila mmoja anautaratibu wake wa kustaafu ila kwa wengine wanaona mbaya na kwasasa ameonyesha kuwa yeye ni kocha mzuri sana
Neema juma
Habari nzuri sana
Frank Patrick
Zizzou zidane maestro kipenz cha Ferguson
Tahiya
Zinedine zedani zizzuu mchezaji aliyeacha historia vichwani mwa wapenda soko hakika alifanya mengi ya kuvutia akiwa uwanjani
Mwanaidi
Alochokifanya Zinedine sio kibaya huo ni uamuzi wake na hakuna mtu wakuweza kumzuia kustaafu japo inasemekana ana rekod mbovu
Mariam mtandama
Vizur
Rehema
Hii ni habari mzuri sn
Antony Luseno
Nakala nzuri hii inatukumbusha mbali
Neema hassan
Asante kwa habari#meridianbettz
Theckla
Zidane atakumbukwa na wengi ktk ulimwengu wa soka
Evaluziga
Nakala hii nzuri inanikumbusha mbali
Khadija
Habari nzuli kwetu mashabiki #meridianbettz
felister
zidane atakumbukwa daima
Elika
Kweli ukitaka kushinda lazima upambane
Rehema Dickson
Kwa uchezaji alio kua nao ni wakiwango kikubwa sana.na kustaafu kwake soka aliona ni sawa na tunajua uwezi kumlidhisha kila mtu umapo fanya jambo lako,ila yeye zidan anatuonesha akua bora tu kwenye uchezaji bal ata kua kocha bado anaonesha kua ni bora zaid
Hope mwaikuka
Kumbe ndo ilvyo
Ester mmakasa
Nilikuwa siyajui haya kwa kusoma makala hii nimeyajuwa sasa.
isha
Zidane tutamkubuka sana maana amefanya mengi
Devotha
Asanteni kwa habari
winfrida
meridian mko vizuri kwa kutukumbusha mambo mbali mbali ya sasa na ya zamani
Adelta
Habari nzuri sana
Dorophina
Tnx meridian kwa update
Ernest
Namkumbuka kwa jina mojaa kali sana Zizzou
Sadick
True Legend of our time#meridianbettz
Amani
True Legend of our time now nikocha Bora barani ulaya big up zizzou#meridianbettz
Samiah
Habari nzuri sana hz
Genia Sikaluzwe
Habari njema Sana hizi
mathayo sonje
huyu ndiye fundi ambaye alikua na vitu vyote, maana anachezea mpira na anafunga pia
Hamidu
Kiungo fundi! Aliyestaff soka akiwa na uwezo mkubwa
mwakalosi
huyu katika ujana wake hakuwa mchezaji hatari lakini uzeewake alikuwa moto
Emmy cleopa
Habar njema
Mwanahamisi
Zidane atakumbukwa daima
Mwajuma
Kiungo mshambuliaji bora
JULIANA
Zidane ni kocha hodari
lombo
gud newz asante
Shafii
Alikua mchezaji mkubwa Sana ulimwenguni ila kwa tukio lile Lilikua ni utovu wa kinidham
Lydia Emmanuel Magoti
Makara mazuri sana
Kenani
Zidane ninmchezaji Bora atazid kukumbukwa licha ya matatzo yake
Aziza mushi
Zidane ni mchezaji mzuri Sana atakumbukwa.
Magdalena
Zidanne aliacha historia nzuri Sana katika mpira na atakumbukwa sana
Caroline
Zidane.long tym sana
Gabriel
Angelos Charisteas kile kichwa alijirusha coz aliamua kumchafulia mkongwe huyo historia
Povel
Zizzou fundiiiii sana