Wachezaji wawili wa mabingwa wa ligi kuu ya Ureno, klabu ya Benfica wameumia baada ya basi la timu hiyo kushambuliwa kwa kupigwa mawe na mashabiki wa timu hiyo.
Tukio hilo linalolaaniwa na wadau mbalimbali wa soka dunia kote, limetokea siku ya alhamisi ikiwa ni baada ya Benfica kucheza mechi yao ya kwanza kabisa kutokea kwenye likizo ya dharula ya ugonjwa wa Corona.
Mashabiki hao walifanya tukio hilo kama ishara ya kuonesha hasira zao baada ya Benfica kutoa suluhu ya bila kufungana na timu inayoshika nafasi za chini kabisa katika msimamo wa ligi hiyo, Tondela.
Matokeo hayo yanawafanya Benfica wabaki nafasi ya pili na alama zao 60 ambazo ni sawa na zile za Porto wanaoongoza msimamo huo, lakini kwa tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa.
Pamoja na kwamba ligi hiyo inaendelea bila ya uwepo wa mashabiki kutokana na janga la Corona, mashabiki hao wa Benfica walizingira uwanja wa timu hiyo ili kuisapoti timu yao hiyo.
Mashabiki wa timu hiyo walilivamia basi hilo kulipiga mawe hali iliyopelekea kuvunja vioo vya basi hilo na kujeruhi wachezaji wawili wa timu hiyo, Julian Weigl na Andrija Zivkovic ambao wamewahishwa hospitali ya Hospital da Luz iliyopo ndani ya jiji la Lisbon.


Salma
Dah!pole kwao
Ester jackson
Kweli mashabiki sio kwa kuipenda timu yao hivyo kisa kuzuiwa kuingia uwanjani wameamua kuwashambulia inabidi wapewe elimu kuhusiana na kutohudhuria kushangilia timu zao kutokana na ugonjwa huu wa corona
Elika
Pole yao
Tahiya
Daah ni tukio mbaya sana mashabiki ni vyema kudhibiti hasira zetu pole kwa majeruhi na timu nzima kwa ujumla
Agness
Duuh hatari Sana pole zao
Mwanaidi
Duuh maskini Benifica ni kweli mashabiki wanahasira lakini hawakutakiwa kufanya hivo kwani mpira huchezwa uwanjani na lolote linaweza kutokea sio makosa yao huenda wao walijipanga vizuri lakini wapinzani wao nao walikuwa vizuri zaidi yao ndio kilichosababisha suluhu
Neema juma
Mmmh inasikitisha kwa kweli.pole yao
Rehema
Aisee pole sn
Antony Luseno
Siku zote timu ikifungwa wanaoumia sana ni mashabiki,kwa tukio hilo walionyesha hisia zao
Neema hassan
Duuuh..pole yao
Theckla
Hasira hasara Sasa wameumiza wachezaji wanategemea nini zaidi ya kufungwa tu
Mariam mtandama
Duuuh
Frank Patrick
Too much fan imotions
Evaluziga
Siku zote timu ikifungwa wanao umia Sana ni mashabiki kwa tukio Hilo wameonyesha isia zao
felister
sad news
Khadija
Duuh polen sana#meridianbettz
Rehema Dickson
Jaman mashabiki wanatakiwa wawe na subra tunajua kama timu yao wanaipenda wajipe muda kwanza ili janga la corona lipite maana ata hao wachezaji pia wanaipenda wakiwa uwanjan na mashabiki pia wawepo ili wawape molali ya kucheza na kuipatia ushindi timu yao
Ester mmakasa
Jamani uongozi unatakiwa uwachukulie hatua hao mashabiki ili iwe fundisho bila ivo sikunyingine wanaweza wakaleta madhara zaidi.
Hope mwaikuka
Sorry for them
isha
Pole sana benfica vipi tuambieni hakuna iliyeumia
Devotha
Pole sana kwa wachezaji wa benfica
winfrida
poleni sana kwa majanga
Adelta
Pole yao
Dorophina
Habari mbaya pole yao
Ernest
Hii Kali, Vyombo vya usalama vinahitajika kuwapa support wachezaji siku hizi wakiwa kwenye usafiri kabla na baada ya mechi
Samiah
Pole yao
Christopher
Pole yao
Hamidu
Duu.!kumbe nako ulaya Kuna mashabiki vichaa…Kama bongo.
mwakalosi
hii ni picha mbaya
Emmy cleopa
Pole yao
Mwanahamisi
Pole yao
Mwajuma
Da kweli mpira umekuwa kama vita
Lydia Emmanuel Magoti
Hii ni picha mbaya sana
lombo
polen sana watu hawatak masihal
JULIANA
Sio poa kabisa
Shafii
Duh nihabali ya kusikitisha sana
Kenani
Wanabolonga Sana tatizo asahv
Aziza mushi
Jamani pole yao.
David Pere
Hao mashabiki wamwfanya vibaya Sana kuwapoga nawe wachezaji wao
Magdalena
Duh habari za kuhuzunishaaa Sana
Povel
So sadππΌππΌππΌ
Theonestina
Pole yao
Amani
Ivi vitendo vinabidi kukemewa si vya kiungwana kabisa
farida ahmadi
Day pole sana