Hispania Dhidi ya Italia Leo Nations League

Timu ya taifa ya Hispania leo itamenyana na timu ya taifa ya Italia leo katika mchezo wa nusu fainali ya kombe la Uefa Nations League utakaopigwa katika dimba la Glorsch Veste.

Timu ya taifa ya Hispania itakwenda kumenyana na mabingwa watetezi wa kombe la mataifa ya ulaya mwaka 2021, Huku mchezo huo ukiwa unatarajiwa kua mchezo mkali na wenye mvuto mkubwa kutokana na aina ya timu zinazokutana.HispaniaTimu ya taifa ya Italia leo watakua wana kazi kubwa ya kufanya dhidi ya Wahispaniola kwani wamekua hawana matokeo mazuri hivi karibuni wanapokutana na timu hivo leo inaweza kua sehemu ya wao kujitetea na kushinda mchezo huo.

kati ya Hispania na Italia leo atakaeshinda atakua ana nafasi kumfuata Croatia katika fainali ya michuano ya Uefa Nations League ambao jana walifuzu fainali ya michuano hiyo baada ya kuifunga timu ya taifa ya Uholanzi kwa mabao manne kwa mawili.HispaniaTimu ya taifa ya Hispania inapewa nafasi kubwa ya kutinga fainali leo katika mchezo huo wa nusu fainali leo usiku, Lakini timu ya taifa ya Italia imekua na kiwango bora sana inapofika katika hatua za mtoano kwenye michuano na leo ni mchezo wa hatua ya nusu fainali.

Acha ujumbe