Gareth Southgate anatarajia kusaini mkataba mpya na timu ya taifa ya Uingereza utakaomuweka mpaka 2024 kwenye michuano ya Euro, mktaba wa sasa unaisha baada michuano ya kombe la Dunia 2022.
Chama cha soka cha Uingereza kinaonekana kukubali masharti na kwa sasa wapo kwenye majadiliano kuhusu mkataba ambao bado Southgate hajaweka saini yake, mkataba wa sasa Gareth Southgate analipwa kiasi cha £3milioni kwa mwaka na inatarajiwa pesa hiyo itaongezka mara mbili kama atasini mkatba huo.

Gareth Southgate alinukuliwa kuwa baada ya michuano ya kombe la Dunia nchini Qatar 2022 angependelea kurudi kwenye mikikimiki ya kufundisha timu za klabu na kulikuwa na shaka kama angepewa nafasi ya kufundisha vilabu vikubwa nchini Uingereza.
Southgate anachelewa kusaini mkataba ambao amewekewa mezani kwa sababu anataka kuhakikisha kwanza anafuzu kwenye michuano ya kombe la Dunia ambayo itakayochezwa mwakani nchini Qatar.
Unawezaje kuikosa hii! njia rahisi ya kutengeneza mkwanja katika kasino maridhawa za meridianbet. Muda wa kufurahia na kutengeneza mkwanja ipo mikononi mwako unasubiri nini?