NAHODHA wa Yanga, Bakari Mwamnyeto amewaita mashabiki wa Yanga kwenye mchezo wa Dabi kesho kwani kutakuwa na sapraiz kubwa kwao.
Akizungumzia maandalizi yao, Mwamnyeto amesema kuwa: “Sisi kama wachezaji tumejiandaa vizuri kuelekea kwenye mchezo wa kesho na morali ipo juu.

“Kutakuwa na sapraiz kubwa kesho hivyo kikubwa tunawaomba mashabiki wajitokeze kwa wingi uwanjani kwa ajili ya kushuhudia.
“Ni kweli kwenye mchezo uliopita wa kirafiki tulipoteza lakini hilo halituumizi kwani tunaenda kupambana na tunaamini tutapata matokeo katika mchezo huo.
“Wachezaji wapya tumewaeleza maana ya mchezo wa Dabi hivyo hata wao wanatamani muda ufike wakacheze ili kupambana jezi ya Yanga hiyo kesho.”

