Klabu ya Inter Milan imekamilisha usajiri wa mchezaji wa kimataifa wa Armenia Henrikh Mkhitaryan kutoka klabu ya AS Roma ambapo kiasi kilichotumika kwenye usajiri huo hakijawekwa wazi.
Henrikh Mkhitaryan amekuwa mchezaji wa kwanza kutoka nchini Armenia kusajiriwa na klabu ya Inter Milan, huku pia akiwa pia mi mchezaji wa kwanza kutoka Armenia kuvichezea vilabu vya Shakhtar Donetsk, Borussia Dortmund, Manchester United, Arsenal, na Roma.

Mkhitaryan aliandika kwenye ukarasa wake wa Twitter “nina furaha sana kujiunga kwenye klabu bora! nitanyafa kwa ubora wangu wote na kujitoa ili kuweza kuisaidia timu kufanikiwa malengo yake.”
Mkhitaryan ameichezea klabu ya AS Roma michezo 117, na amefanikiwa kufunga magoli 29 na kusaidia 28, huku akiichezea Armenia michezo 95, na kufunga magoli 32.
ALIYA’S WISHES
Bila shaka unatamani ushindi mkubwa, vipi kuhusu kujaribu Sloti hii ya Aliya’s Wishes? jaribu ushinde sasa.

