Aziz Ki Amkosha Nabi Yanga

KOCHA Mkuu wa Yanga, Nassredine Nabi amefurahishwa na viwango vya wachezaji wapya ndani ya kikosi hicho akiwemo pia, Stephane Aziz Ki.

Yanga ambayo imeweka kambi Avic Town inaendelea na maandalizi ya msimu ujao wa 2022/23.

Wachezaji wapya ndani ya kikosi cha Yanga ni pamoja na Benard Morrison, Joyce Lomalisa, Lazarious Kambole, Gael Bigirimana na Stephane Aziz Ki.

Akizungumzia kambi yao, kocha Nabi amesema kuwa mazoezi yanaendelea vizuri na amefurahishwa na viwango vya wachezaji wake kwenye mazoezi hayo.

“Nimefurahi kwa ambacho nimeona kwa siku hizi ambazo tumefanya mazoezi hata kama kuna wachezaji ambao wanakosekana kwenye kikosi.

“Lakini pia nimefurahi kutokana na wachezaji kuwa fiti kwani wamefuatilia ileprogramu niliyowatumia walipokuwa likizo na pia nimefurahi kuona wachezaji wapya ambao wamesajiliwa kwenye kikosi kuwa fiti.”

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.