Amos Makalla Atembelea Mo Simba Arena

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla leo ametembelea Uwanja wa Mo Simba Arena uliopo Bunju.

Makala ameruhusu uongozi wa Klabu ya Simba kuendelea na mradi wa ujenzi wa ukuta kuzunguka eneo hilo ukiwa ni mpango kazi wa ujenzi wa viwanja vya michezo.

Aidha kiongozi huyo amewaagiza watu waliovamia eneo hilo kuhama ndani ya siku 60.
Pia mkandarasi wa ujenzi wa ukuta huo kwenye uwanja wa Mo Simba Arena tayari amefika eneo la kazi kwa ajili ya kuanza ujenzi.

Kwa mujibu wa Mtendaji Mkuu wa Simba, Barbara Gonzalez ameweka wazi kuwa malengo makubwa ya timu hiyo ni kuwekeza katika eneo la uwanja kwa kuwa na viwanja vya nyasi bandia na asilia.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.