Dortmund Wanamtaka Naby Keita

Borussia Dortmund wanaripotiwa kuendelea kumfuatilia kiungo wa Liverpool Naby Keita kwa uwezekano wa uhamisho wa bure msimu ujao.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Guinea ameingia mwaka wa mwisho kwenye mkataba wake Anfield na tayari ameshakusanya vilabu kadhaa maarufu barani Ulaya.

 

Dortmund Wanamtaka Naby Keita
Naby Keita

Hata hivyo, Dortmund ya Edin Terzic inaonekana kuwa mstari wa mbele katika kuinasa saini ya Keita baada ya hivi karibuni mchezaji huyo kudai kuwa hana uhakika juu ya mustakabali wake nchini Uingereza.

Kulingana na Sport Bild, Keita ni mmoja wapo ya vipaumbele vya juu zaidi vya Dortmund katika dirisha lijalo la usajili huku wakipania kuimarisha safu yao ya kiungo.

Mazungumzo kuhusu mkataba mpya yanaendelea kati ya Keita na Liverpool, hata hivyo vilabu vingine vinavyomtaka mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 vinaweza kusimamisha majadiliano.

Dortmund Wanamtaka Naby Keita

Kiungo huyo bado hajacheza kwenye kikosi cha Jurgen Klopp msimu huu kutokana na jeraha la misuli ya paja ambalo ndilo la hivi punde katika orodha ndefu ya matatizo ya utimamu wa mwili.

Keita amekosa mechi 72 katika misimu yake minne kamili, katika klabu hiyo huku akisumbuliwa na majeraha ya kifundo cha mguu, na nyama za paja mara kwa mara.

Tangu alipowasili kutoka RB Leipzig mnamo 2018, Keita ameshinda Ligi ya Mabingwa, Ligi Kuu, Kombe la FA na Kombe la Carabao akiwa na Liverpool, huku akiwa amecheza mechi 117, lakini hana uhakika wa kuanza wakati kila mtu anapatikana.

 

Dortmund Wanamtaka Naby Keita
Mo Salah akishangilia na Keita.

Liverpool wana chaguo la kiungo akiwemo Fabinho, Jordan Henderson, Thiago, Curtis Jones, James Milner, Arthur Melo na Alex Oxlade-Chamberlain, pamoja na chipukizi Harvey Elliott na Fabio Carvalho.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.