Uhamisho Jadon Sancho ni Gombania Goli

Jadon Sancho, 20, ametajwa kuwa anataka kurejea Ligi Kuu ya Uingereza baada ya kuondoka huko mwaka 2017. Alitokea Manchester City kwenda kukipiga Bundesliga akiwa na Borrusia Dortmund hadi leo. Kwa msimu wa 2019/2020 amecheka na nyavu mara 14 na kutoa asisti 15.

Tangia aondoke Manchester City kwenda Ujerumani ni kama alipiga hatua kubwa zaidi na uwezo wake umewavutia klabu nyingi Ulaya, zikiwepo kadhaa kutoka EPL, na mpaka sasa mipango ya nani apate nani amkose inachezeshwa mezani! Hapa tunagusa kidogo klabu zinazomfukuzia kiasi cha kufanya usajili wake uwe kama gombania goli, atakayempata ndiye huyo mshindi!

Manchester United

Manchester United wanataka kumsajiuli Jadon Sancho dirisha la usajili litakapofunguliwa. Wakati huo bosi Ed Woodward ameonya kuwa mambo hayatakuwa kama yalivyozoeleka kwenye uhamisho wa sasa.

Lakini ukweli ni kuwa United wanataka kufanya lolote linalowezekana kuboresha safu ya ushambuliaji kuelekea msimu ujao na Jadon Sancho ni moja ya karata wasiyotaka kuipoteza.

Chelsea
Bila shaka, hakuna kitu mashabiki wa Chelsea kitawasuuza mioyo yao kama kumuona Jadon Sancho ametua klabuni hapo msimu huu wa joto! Chelsea pia wamehusishwa kuingia kwenye kinyanga’anyiro cha kuinasa sahihi ya kinda huyu kutoka Dortmund.

Frank Lampard na kikosi wanajitahidi kuona namna bora ya kumnasa. Kinda huytu ameenda kuwa bora zaidi ya baadhi ya wachezaji wa Chelsea ambao amewahi kucheza nao, sasa wanataka aongeze nguvu kikosini.

Liverpool

Liverpool wamekuwa wakihusishwa na Jadon Sancho, beki wa Liverpool Alexander Anorld alinukuliwa akisema kuwa itakuwa poa sana kama staa huyu akitimba kwa majogoo, anaamini kikosi chao kitakuwa bora zaidi na kwake binafsi itakuwa poa zaidi.

Sancho ameweza kumjibu Anold kupitia ukurasa wake wa Instagram, na huenda akawa amewaacha na matumaini Liverpool baada ya kuchapisha macho mara 4 alipokuwa anahusishwa na kuhamia Liverpool na Alexander Anorld ikiwa ni ishara kuwaa anaweza kuwa anafahamu jitihada za chini ya kapeti.

Sio EPL tu!

Hata hivyo sio vilabu vya EPL tu vinavyowinda sahihi ya Jadon Sancho. Barcelona pia wametajwa kuwa wanaisaka sahihi yake na anaweza kuwa mbadala wa Neymar klabuni hapo.

11 Komentara

    Kizuri kinajiuza Mana jadon Sancho ni mchezaji ambaye anaonyesha jitihada za Hali ya juu pindi anapokuwa uwanjani

    Jibu

    Mchezaji mzuri sana

    Jibu

    Nenda man u sancho.

    Jibu

    Aende man united😋

    Jibu

    Mchezaji hatarii hatarii

    Jibu

    Namkubali mchezaji mzuri nayupo vizuri azidi kulisongesha kabambe

    Jibu

    Uje England tu

    Jibu

    Bora aje man u

    Jibu

    Huyu bora abaki huko ujeramani au aende spain tu asirudi uingereza

    Jibu

    Yupo vizur

    Jibu

    Bora aje man u

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.