Maswali Mazito kwa Lewis Hamilton na F1

Ni wakati mgumu sana ambapo wachezaji wameweza kujiuliza hatma zao katika michezo yao wanayoshiriki. Mmojawapo ni Bwana Lewis Hamilton ambapo mshindi huyo mara sita wa ubingwa wa dunia siku ya Jumapili alikiri kuwa amewaza sana juu ya hatma yake ya michuano ya Formula 1 wakati huu ambapo dunia imekumbwa na janga la Corona.

Amekuwa akihangaika sana kurudi katika hali ya ushindani kimchezo. “Kuna siku ninaamka nikiwa mwenye mawazo sana. Sioni haja ya kuendelea na mchezo wangu huu, tunaenda wapi? Nini kitafuatia? Niendelee kuendesha magari na kushiriki mbio za magari?”

Hayo ni maswali ambayo mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 35 amekuwa akijiuliza mara kwa mara. “Ninawaza juu ya haya mambo mengi sana, na kuishia kusema acha liwalo likawe tu. Na saa moja linalofuatia likiisha, ninasema tena, acha iwe. Ninapenda ninachokifanya. Na siwezi kusimama kushiriki mbio za magari.”

Msimu huu Hamilton anategemea kuifikia rekodi ya mwenzake Michael Schumacher aliyetwaa mataji saba ya dunia.

Hata hivyo, amekuwa hajui nini kitajiri kutokana na kusambaa kwa ugonjwa wa Coronavirus. Kutokana na jambo hilo mbio 10 zimesimamishwa na kuahirishwa kuendelea kwake.

Msimu mpya hautaanza mpaka pale ikifika tarehe 5 Julai nchini Austria endapo itawahi sana kuanza.

“Ni suala la kujiweka sawa kiakili. Ni namna ya kuangalia unajipenda zaidi wewe mwenyewe,” aliongezea Hamilton akiongea wakati wa Mental Health Awareness Week.

“Unatakiwa kujipenda zaidi na kuwa huru kwako mwenyewe.” Aliongezea: “Endapo hatujifunzi kitu wakati huu wa matatizo basi tujiulize ni nini tunachokifanya? Tunakuwa tunapoteza muda tukikaa bila ya kufanya kitu.”

Unadhani Hamilton ataikacha langalanga?

31 Komentara

    ni muda wa kuishi nao huu ugonjwa maana sio ugonjwa wa kwanza kuna Spanish flu iliuwa watu wengi sana

    Jibu

    Ni kweli lazima ajiulize maswali mengi ila sio yeye tuu ni watu wengi sana wamejiuliza sababu imewafanya warudi nyuma na kuyumba sababu ya huu ugonjwa hatatishi ila hizi ni changamoto kama chanagamoto nyengine kwenye michezo na mambo mengine ni suala la kumuomba sana mungu aepushie mbali na hali irudi kama zamani

    Jibu

    Ugonjwa wa corona umeharibu mipango mingi sana lakini haina budi kuishi nao maana kuna mda tutasahau majanga na matatizo yote tuliopitia

    Jibu

    Kwer nimaswali magumu na majibu yke ni fumbo kubwa mana hakuna anayejua huu ugonjwa utadumu kwa muda gani

    Jibu

    Hiki ni kipindi cha mpito kikubwa kuomba mungu huu ugonjwa wa corona uishe..

    Jibu

    Maswal lazima yawe mengi coz janga hili la corona lebadilisha mambo mengi sana michezo imesimama na ndo ajila,, familia inamtegemea na mambo mengine mengi ila mungu atafanya wepesi kila kitu kitakua sawa tu

    Jibu

    Duuuh

    Jibu

    usikate tamaa lewis ni mambo ya mapito kila kiyu kitakaa sawa na utarudi mchezoni

    Jibu

    Hiki ni kipindi kigumu Sana kwa ajili ya huu ugonjwa wa corona Cha msingi kuomba mungu atuepushe

    Jibu

    Endapo hawatajifunzi kitu wakati huu wa matatizo basi wajiulize ni nini wanachokifanya? Tunakuwa tunapoteza muda tukikaa bila ya kufanya kitu.”

    Jibu

    Mmmmh! Jamani don’t give up Lewis

    Jibu

    Jamani Hamilton anapenda sana kazi yake #Meridianbettz

    Jibu

    To be honest huu ugonjwa umeharibu kila ktu kwenye taratibu zetu

    Jibu

    Maswali lazima yawe mengi sababu janga hili la Corona michezo imesimama Yani Ila mungu atafanya wepesii Mambo yatakaa sawa.

    Jibu

    Huyu jamaa atatetea nafasi yake maana hakuna wa kushindana naye akiwa kwenye mashindano

    Jibu

    Hamilton Lewis bonge la dereva kwny mbio za magar

    Jibu

    Hamilton ni tishio kwa sasa ulimwenguni

    Jibu

    Aikache tu akapate challange nyingine na uongozi mwingine

    Jibu

    Hawezi kuikacha langalanga na kuhusu covid 19 n jangw lisiloisha hvyo inabid tuishi nalo na mambo mengne yaendelee

    Jibu

    Hamilton yuko vizuri sana namkubali huyu jamaa

    Jibu

    Duuuh!! Ila usikate tamaa lewis

    Jibu

    Duh asikate tamaaa aombe mungu tu

    Jibu

    Hatar sana aisee

    Jibu

    Sema huo Mchezo ni atari

    Jibu

    Ili gonjwa limetibua kila kitu Ila tu tuishi nalo kwa tahadhali

    Jibu

    Lazima tupate of huu uhonjwa unatisha sana kikubwa zaidi hauna kinga..!ni mwenyew tu kua makini lakini hauwezi kuukwepa na itachukua mda sana kuusahau

    Jibu

    Ni suala la kujiweka sawa kiakili. Ni namna ya kuangalia unajipenda zaidi wewe mwenyewe

    Jibu

    Daaah ili gonjwa lipite tu kwakwer

    Jibu

    Ugonjwa huu unawatia hofu watu wengi

    Jibu

    Mungu atusaidie huu ugonjwa uishe dunian maana bado tunaogopa sana.

    Jibu

    Daaaah hatari corona siyo poa

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.