Kylian Mbappé Atakuja Kukumbukwa Kwenye Vichwa vya Wafaransa?

Mbappe ana mtihani kama wa Obama jioni ile ya 2008 pale Chicago, safari ya mtoto huyu ilianzia pale visiwani Monaco kwenye dimba la Stade Louis, aliwastua Wafaransa, alibisha hodi kwenye lango kubwa la historia ya soka lao

Nachotaka kuwaambia ni kuwa taifa lile halina tabia ya kuwapamba sana watu waliofanya makubwa kwenye soka lao, sahau kuhusu Raymond Kopa, Thierry Henry na Michel Platin, hawa wote licha ya ubora wao hakuna hata mmoja aliyepewa heshma ya sanamu (statue) watu mioyo yao ya baridi tu

Mbappe

Sanamu pekee ni la Zinadine Zidane, ilimchukua muda msanifu Abdel Abssemed kuliandaa, lakini sio kwamba ni sanamu la kumsifu mtoto wa mitaa ya La Castallane, Marseille bali ni sanamu la kuwakumbusha vizazi kuwa Zidane alifanya ujinga kumpiga Matterazzi kichwa, tukakosa kombe kwa ujinga wake

Nageuka kuitazama miguu ya Mbappe, najaribu kuwaza atabadili upepo huu?? Ataweza kujengewa sanamu bora kukumbusha vizazi juu ya ubora wake??, Nafikiria mchezaji wa kwanza kinda kufikisha mabao 15 UEFA, nafikiria ni mchezaji wa kwanza wa akiba kupiga hatrick UEFA

Nafunua tena ukurasa nagundua licha ya miaka yake 21 ni mchezaji ghali namba mbili duniani, naendelea kufahamu kuwa ni kinda wa pili baada ya Pele kuingia kambani kwenye fainali za kombe la dunia, bado nawaza alikuwepo sehemu ya kikosi cha mastaa ila alidhihirisha ubora wake

Bado nawaza mabao yake 90 kwenye mechi 120 za PSG na assists 49 naona kuna kitu, naiona tena historia ya Mwafrika kwenye historia ya taifa kubwa kama Ufaransa, akifika miaka 28 naamini sanamu litakuwepo pale Paris! Tuombe uzima

50 Komentara

    Watamkumbuka sanaa kwa mambo aliowafanyia,na history aliyoiweka

    Jibu

    Mbappe anaweza kumrith zinadane kama ataendelea na uwezo wake

    Jibu

    Mbappe atafata nyayo za zidane

    Jibu

    nagundua licha ya miaka yake 21 ni mchezaji ghali namba mbili duniani, naendelea kufahamu kuwa ni kinda wa pili baada ya Pele kuingia kambani kwenye fainali za kombe la dunia Ni historia pia bado anazidi kuweka history

    Jibu

    Ahsante kwa taarifa

    Jibu

    Mbappe akijitahidi atamrithi zidane

    Jibu

    Mbappe Ni mchezaji mzuri lazima haache historia kwa mpira wake mzuri

    Jibu

    nafikiri ni mambo mengi ameweza kuyafanya lakini mpaka kukaa akilini mwa watu lazima afanye jambo lakipekee; kama la zizu, maana kumpiga mtu kichwa kama kile ”aiseee!!!!” si jambo la kawaida

    Jibu

    Mbappe the best player France and Europe

    Jibu

    History ameweka bado akiwa mdogo na haitafutika milele na watamkumbuka kwa mengi hususani kwenye timu ya taifa

    Jibu

    Amekuja na majabu meng kweny soccer lake lazma awakae watu kichwan

    Jibu

    Mbappe yupo vizuri razima haonyeshe mahajabu kuwakaa watu vichwani lazima kwasababu anajua nn anakifanya huyo jamaa anakubalika

    Jibu

    Mbappe mpambanaji hanayejiamini..!hatajenga history yake

    Jibu

    Makala nzuri sana , nimependa ulivyomchambua kijana huyu machachali kwenye soka ambapo napata mashaka kama angekuwa muingereza hiyo promo yake sasa.

    Jibu

    huyu kijana anaonekana ni hatari kulingana na ligi anayocheza ligi ya ufaransa ni moja ya ligi nyepesi sana sikushangaa chamakh kutoka kuwa mfungaji bora ufaransa kwenda arsenal sasa kiande cha mwisho

    Jibu

    Mbappe ni mchezaji mzuri tena bado kinda na ili kuonyesha yeye ni bora achezee ligi tofauti kuonyesha ubora alioonyesha akiwa Monaco na PSG. Ronaldo ameonyesha ubora wake katika ligi tofauti#meridianbettz

    Jibu

    Mbappe ni mchezaji mwenye umri mdogo lakini ni mchezaji mahiri sana hasa akiwa uwanjani lazima wamkumbuke

    Jibu

    Mbappe ni mchezaji bora sana kwa upande wangu..nategemea ataweka historia katika soka

    Jibu

    Mbappe ni mchezaji mzur na kiumri bado anasafar ndefu ya kufika mbali sana katika soka natumai atajengewa sanamu muda ukifika

    Jibu

    Mbappe anajua sana

    Jibu

    Mbappe mchezaji ambae hatasahaulika ujerumani hata kama wasipomjengea sanamu

    Jibu

    Mbappe mchezaji mzuri sana ,ingekuwa sahh angejengewa sanamu iwe kumbkumbu ya kudumu kwa vizazi vijavyo..

    Jibu

    Asante kwa taarifa meridianbet #

    Jibu

    Sana atakumbukwa kwa uwezo wake wa kujitoa kwa kupiga mpira na kujituma bila kujal umri wala tim kubwa kiasi gan anayocheza nayo ameonesha juhudi kubwa ni jambo zuri la kuigwa na vijana wanao chipukia katika soka hongera sana mbappe utafika mbali sana zaidi ya ulipo now

    Jibu

    Mbappe Ni mchezaji mzuri pia bado mdogo na ili kuonyesha yy Ni Bora zaidi acheze lingi tofauti kuonyesha ubora wake!

    Jibu

    lazima akumbukwe tu mbappe ni mchezaji mzuri

    Jibu

    Mbappe kawa gumzo #Meridianbettz

    Jibu

    Asante kwataharifa

    Jibu

    Eeh kikubwa uhai

    Jibu

    Mbappe ni mchezaji mzuri lazima aache historia

    Jibu

    Kwa Mbappe bado mno anahitaji juhudi za ziada maana kuna kawaida ya wachezaji wadogo kulewa hela wanazopata

    Jibu

    Talent player#meridianbettz

    Jibu

    Mbappe mchezaj mzur Sana hv sasa ulaya na dunia

    Jibu

    bonge la makala ahsanteni meridian

    Jibu

    Mbappe namwamini zaidi coz ni kijana anayejitambua na anajua anachokifanya lazima aache historia

    Jibu

    lakini akihitaji tuzo kubwa yamfaa aende Liverpool Madrid or Barca

    Jibu

    mchezaji ghali namba mbili duniani, naendelea kufahamu kuwa ni kinda wa pili baada ya Pele kuingia kambani kwenye fainali za kombe la dunia## meridianbettz

    Jibu

    Mbape yuko vizuri Sana anapokua dimbani anapambana kweli

    Jibu

    Kweli kabisa

    Jibu

    Mbappe ni Yuko vizur Sana

    Jibu

    Mbappe anaweza kumrithi zidane
    Kama akiongeza juhudi

    Jibu

    Mbappe atachukuwa mikoba ya zidane

    Jibu

    Mbappe yupo vizur nafikili anaweza akamvuka hata zidane

    Jibu

    Mbappe namkubali sana

    Jibu

    Noma sanaa huyo dogo

    Jibu

    Mbappe tangu nilivoanza kumsikia mpaka leo bado yuko vizuri sana yaani hashuki daraja.

    Jibu

    Yuko vizuri.

    Jibu

    Bado ana muda zaidi wa kuonyesha ubora wake pale ufaransa

    Jibu

    Asante kwa taarifa

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.