Klopp Huwezi Tamba Zaidi ya Miaka Minne

Bella Gutaman, gwiji fulani wa Benefica aliwahi kusema “mfumo au falsafa haiwezi kutamba kwa zaidi ya miaka minne.” Gutaman alisema hivo kwasababu anaamini mfumo wako unapofanya vizuri, timu pinzani zinaumiza kichwa kukusoma na suala la muda tu kabla hawajapata mbinu za kukuvuruga.

Liverpool chini Jurgen Klopp, imeishi kwa kutegemea ubora wa wachezaji watano kuwapa magoli. Mabeki wawili wa pembeni na washambuliaji watatu. Wanategemea zaidi kupita pembeni na kutengeneza nafasi kutokea pembeni. Kazi kubwa ya viungo wa Klopp ni kukaba mpira na kuuepekela pembeni, huko ndipo mabao yanapopikwa. Usishangae ukiambiwa ‘full backs’ wa Liverpool wanaongoza kwa assist ndani ya Liverpool.

Kwa falsafa hii, Liverpool wamebeba taji la ligi(EPL) na Ulaya(UEFA). Kama uliwatazama Liverpool walipocheza na Leeds mchezo wa ufunguzi, nadhani uliona namna vijana wa Marcelo Biesla walivopambana kuwazuia mabeki wa pembeni wa Liverpool. Na hii inakuwa mara ya kwanza Liverpool kufunga mabao 3+ bila beki wao yoyote wa pembeni kutoa assist kutoka kwenye mchezo wa wazi (open play).

Hii inamaanisha nini? Huenda ukawa mwisho wa ujanja wa Klopp kushinda kirahisi kutokea pembeni. Ameshatesa sana na hii falsafa, sasa ni muda wa kubadilika na kujaribu kitu kingine kipya.

Hiki kitu kipya anakuja nacho Thiago Alcantara, kwa muda mrefu Liverpool haijawa na viungo wabunifu na wamiliki mpira. Labda ndio sababu iliyomfanya Klopp ategemee zaidi upishi kutokea pembeni kuliko katikati. Uchezaji wa Thiago unakuruhusu kupita katikati ya uwanja. Ni aina ya mtu anayejua kusambaza mpira. Japo hatakupa sana pasi za mwisho, ila atakufikishia mpira hadi mpigaji wa pasi ya mwisho. Nadhani ni muda Klopp anaenda kubadilika na kujaribu kucheza katikati ya uwanja zaidi ya pembeni.

Thiago ataitoa timu nyuma ataifikisha mbele, wale washambuliaji watatu wa mbele watakuwa na kazi mbili. Kwanza kutengenezeana nafasi na kufunga. Hii itampa ahueni Firmino, aliyelazimishwa kushuka chini ili aisaidie timu kucheza. Ndiyo maana alikaukiwa mabao msimu uliopita. Kwasababu Thiago atakuwa mchezeshaji, yeye atabaki juu na jukumu lake mama la kufunga na kupika mabao.


SHINDA NA MERIDIANBET!

Tengeneza pesa kidijitali kwa kubashiri mbio za farasi hapa Meridianbet! Chagua nani ashinde, unakusanya mkwanja.

Cheza Sasa.

39 Komentara

    Habari njema

    Jibu

    hayo ni maneno tu wanamkatisha klopp tamaa

    Jibu

    Thiago amekuja kufanya mabadiko Liverpool msimu huu

    Jibu

    Liver lazima na msimu huu wabebe hizo Ni hisia za wapenzi watazamaji hazitasaidia chochote

    Jibu

    Thiango anajituma sana

    Jibu

    Wanamkatisha Kropp tamaa ila akipambana anaweza

    Jibu

    Klopp yupo vizuri sana hanambinu nyingi

    Jibu

    Mpira ni sayansi ya mbinu na falsafa ya Pep Guardiola haijawahi kubadilika na anapata matokeo mazuri#meridianbettz

    Jibu

    Klopp ni kocha mzuri sana

    Jibu

    Ni kocha mzuri sana klopp

    Jibu

    Mtazamo wa Gutaman upo sahihi sana na ni wa kuheshimiwa

    Jibu

    anamaanisha mfumo anaotumia klopp sio mzurii

    Jibu

    Klopp yuko vzuri

    Jibu

    Ni kocha mzuri sana klopp#Meridianbettz

    Jibu

    Klopp yuko poa

    Jibu

    Ni kocha makini sana

    Jibu

    Klopp Ni kocha mzuri@meridianbettz

    Jibu

    Ngoja tuone mwisho wake

    Jibu

    Kwa ligi ya uingereza kutamba miaka miwili ni kitu kigumu sana

    Jibu

    Klopp anajua anachokifanya

    Jibu

    Klopp ni kocha mzuri

    Jibu

    Klopp yupo vzr#meridkanbettz

    Jibu

    Yote yanawezekna Ila akipambana anatamba tu hata miaka kumi

    Jibu

    Ni ngum epl ligi ya ushindan

    Jibu

    Kwa kocha kufanya vizur Kwa mda mlef team moja ngum

    Jibu

    Good news

    Jibu

    Anajua

    Jibu

    Ngoj tuone final itakuwaje

    Jibu

    Klopp yuko vizuri

    Jibu

    Namkubar

    Jibu

    Kwa ligi ya uingereza kutamba miaka miwili ni kitu kigumu sana

    Jibu

    klopp yupo vizuri sana ila kila kukicha anabidi abuni mbinu mbadala kwa ajili ya timu

    Jibu

    Ni kweli kabisa

    Jibu

    Hata ivyo amefanya mambo makubwa kwa kila klabu aliyofundisha

    Jibu

    Bado yupo vizuri

    Jibu

    Epl ni iigi ya upinzan kudum na title mfululizo haliwezekan

    Jibu

    Klopp yupo vizuri inabidi aendelee kukaza

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.