Arsene Wenger aliwahi kusema zipo njia mbili tu za kutengeneza timu imara ya ushindani. Ya kwanza ni kuwekeza katika kukuza vijana na ya pili ni kumwaga pesa kununua waliokwisha kutengenezwa. Njia zote hizi zinafanya kazi lakini hazifanani.
Njia ya kwanza inahitaji uvumilivu na mipango ya muda mrefu sana. Ndiyo sababu timu nyingi zimepiga chini huu mpango. Wanachagua tu kujitosa sokoni na kutengeneza timu imara. Ndivyo pesa inavyoendesha dunia. Kuanzia kwa Real Madrid iliyotwaa UEFA tatu mfululizo mpaka kwa PSG na Bayern Munich zinazocheza ligi zao binafsi, zimeundwa kwa pesa tu. Hakuna kingine!
Kwa Manchester United, kabla ya kuilaumu mikono ya David De Gea, kabla ya kuzihoji mbinu za Ole Gunner Solksjaer, kabla ya kuzituhumu kosakosa za Antonio Martial, nadhani anatakiwa kutazamwa Mkurugenzi Ed Woodward na ‘sekretarieti’ yake. Kwa walipoishia Man United msimu uliopita, ni wazi walihitaji sura mpya kikosini ili kupiga hatua zaidi. Walihitaji marekebisho baadhi ya maeneo ili kuwa washindani zaidi.
Sahau kuhusu ulinzi, kule mbele wanahitaji washambuliaji wawili hatari (siyo machachari), watu kama Harry Kane na Jadon Sancho. Katikati walifanya vizuri kumuongezea Bruno msimu uliopita na ujio wake umelipa, tayari wanayo Pogba, Fred, Mctominay na Matic. Kwa maoni yangu nadhani katikati hawahitaji mtu ukizingatia wamemsajili Donny Van Beek. Wanahitaji beki mmoja wa kati wa kusimama na Maguire na beki mmoja wa kushoto. Hao tu.
Hayo maelezo niliyoweka hapo juu, nimerudia tu alichokisema Ole mwisho wa msimu uliopita alipozungumzia marekebisho atakayofanya kikosini. Ajabu ni kuwa hajayafanya mpaka sasa. Unadhani shida ipo wapi? Shida siyo Ole, shida ni mtu anayesimamia fedha, Ed Woodward. Hakuna kocha asiyetaka kusajili, hakuna kocha asiyetaka kushinda. Kama Ole aliona madhaifu yote hayo, ina maana alihitaji kuyarekebisha. Atarekebisha vipi bila pesa ya usajili?
Crystal Palace walivoshuka Old Trafford jana bila uwoga, Man Utd inahitaji kufanya kitu kabla dirisha halijafungwa kama kweli wanahitaji taji la ligi kuu.
SHINDA NA MERIDIANBET!
Tengeneza pesa kidijitali kwa kubashiri mbio za farasi hapa Meridianbet! Chagua nani ashinde, unakusanya mkwanja.
Tatu
Maneno aliyosema arsene wenger ni mnzuri Sana vilabu vingi vingefuta mfumo wake wala wasingepoteza pesa nyingi kwenye usajili
Zeiyana
Ukingalia ni kweli man chester wanaitaji wachezaji machachali na wanao jituma sain ya Sancho ndio ingekua bola kwao
Dorophina
Wenger yupo sahihi kwa alichokiongea man u kwa sasa inahitaji kikosi kizuri na watu wanaoujua mpira vizuri ili kuiinua klabu
Lydia Emmanuel Magoti
Nikweli man wanaitaji wachezaji wenye kujituma na wenye judi zakupambana kwaio inabidi wafanye usajiri kwaraka kabla dirisha alija fungwa wa pate majembe wenye amsha masha ya timu
Devotha
Man United bado wanakikosi kibovu tu
Sadick
Ferguson alipata mafanikio makubwa hata wakati timu haikuwa na wachezaji wazuri sana alijua namna ya kuwapa motisha na kufuata game plan. kwa sasa Man U tatizo ni kocha pia#meridianbettz
Rehema
Asante kwa taarifa
jullie
habari nzuri
Antony Luseno
United wasipo pata ufumbuzi ni wapi wanafeli itawagharimu ata zaidi ya miaka 15 pasipo kuchukua kombe la EPL
caroline
man u wanatafuta wa kumtupia lawamaa
Nasra
Man u wajipange upya
Mwajumah
Man u bado wanakikosi kibovu sana wasitafute mtu wa kumpa lawama#Meridianbettz
Sauda
Man U wanatakiwa kuimarisha kikosi
Janeflora malisa
🔥🔥
felister
man kwa sasa imekua jumba bovu
Ernest
Old Traford patachimbika pale we subiri
aisha
United inabid isajili washambuliaj makin wa kutupia ili isake ubingwa tena
Hidaya
Man u wajipange upya waangalie wapi walipokosea
Gabriel
vilabu vingi vingefuta mfumo wake wala wasingepoteza pesa nyingi kwenye usajili
Khadija
Asante kwa nakala#meridianbettz
Hopemwaikuka
Na hii ndio sababu ya kufkr kabla ya kutenda
Issa
Ole ana kikosi imara sana ila mbinu tu aongeze
Amiri Kayera
Man U sijajua tatz wapi
Povel
United wamestail walichokipata ukiangali ah mchezo wa jana wamecheza chin ya kiwango wachezaj wote wanapaswa kulaumiwah
Neema
Man U kikubwa kukaa kutuliza kichwa kwanza
Theonestina
Man mnatuangusha Sana bwana
Elika
Man waimarishe kikos
David Pere
Ferguson alipata mafanikio makubwa hata wakati timu haikuwa na wachezaji wazuri sana alijua namna ya kuwapa motisha na kufuata game plan. kwa sasa Man U tatizo ni kocha pia
magdalena
wenger alikuwa anatazama mbali sana
warda
Swala la kukuza vijana ndo muhimu sana#Meridianbettz
Fatina mfigi
Man u wanatuangusha
Flomena
Good news
Mwanahamisi
Man u wajipange
Salma ngende
Man u bado wako vibaya
Zahara omary
Sijui man wanakwama wapi siku hiziii
Shan
Ni umakin tu na kufanya usajili kwa fowad matata tu na idara ya ulinz
Sabrina
Man u wanatakiwa wajipange wana kikosi kibovu