Kagere Hatihati Novemba 7

Mfungaji namba moja ndani ya Bongo kwa misimu miwili mfululizo akiwa amefunga jumla ya mabao 49 ambapo alifunga mabao 23 msimu wa 2018/19 na mabao 22 msimu wa 2019/20 na mabao manne msimu wa 2020/21 Meddie Kagere kuna hatihati akaukosa mchezo dhidi ya Yanga, Novemba 7 kutokana na kusumbuliwa na majeraha.

Kagere ana zali la kuwafunga Yanga ambapo kwenye mabao yake hayo 49 mawili aliwafunga Yanga, aliwafunga bao moja msimu wa 2018/19 Uwanja wa Mkapa wakati Simba ikishinda bao 1-0 na kipa alikuwa ni Ramadhan Kabwili na aliwafunga 2019/20 kwenye sare ya kufungana mabao 2-2 na kipa alikuwa ni Faroukh Shikhalo.

Kwa sasa dabi hiyo ya Kariakoo imebakiza siku 18 na Kagere yupo chini ya uangalizi akitibu majeraha yake aliyoyapata Oktoba 4 Uwanja wa Jamhuri, Dodoma wakati Simba ikishinda mabao 4-0 dhidi ya JKT Tanzania na yeye alitupia mabao mawili.

 Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara amesema kuwa kikosi cha Simba kipo vizuri huku kikiwa na wachezaji wachache majeruhi waliopo chini ya uangalizi maalumu.

“Gerson Fraga anaedelea vizuri na John Bocco ameanza mazoezi mepesi. Pia Meddie Kagere ambaye kwa ukweli yeye atakuwa nje kwa muda wa wiki tatu kwa mujibu wa jopo la madaktari mpaka pale hali yake itakapotengemaa atarejea uwanjani.

“Matarajio yetu ni kwamba Wanasimba wataendelea kuwaombea wachezaji wetu ambao ni majeruhi ili warejee kwenye afya zao,” alisema Manara.

Wiki tatu ambazo ni siku 21 zinamfanya Kagere kutokuwa na uhakika wa kuivaa Yanga, Novemba 7 kwa kuwa anaweza kuwa fiti Novemba 6 huku mechi dhidi ya Yanga ni Novemba 7 jambo ambalo linaleta ugumu kwake kuanza kwenye mechi hiyo ambayo inatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa.


Ondoka na Mkwanja Kwenye Tsh. 160,000,000

Hii ndiyo burudani yenye ushindi! Ingia kwenye kasino ya Meridianbet kufukuzia ushindi huu.

Soma Zaidi

29 Komentara

    Kagere hata awepo tareh 7 aijalishi kichapo kitawahusu wana msimbaz tu

    Jibu

    Mungu atamsaidia atapona

    Jibu

    Kagera wako vzur sana 👍

    Jibu

    Vizur

    Jibu

    Kagera jembe

    Jibu

    Kagera uko vzr

    Jibu

    Asapo kuwepo fresh tu kuvuja kwa pakacha

    Jibu

    Get well soon. MAMBA mk14🙏🏼🙏🏼🙏🏼🙏🏼

    Jibu

    Kwan mchezaji ni yeye tu

    Jibu

    Janja janja ya tu ya Simba hiyo

    Jibu

    Simbaaaaa wakali

    Jibu

    Pole yake kagere simba inapengo la mfungaji mzuri katikati ya uwanja

    Jibu

    dah itakuwa bonge la pengo kwa wana simba ila atakuwa sawa hivi karibuni

    Jibu

    Getwell soon

    Jibu

    Ukiangalia pale clabuni simba hawana mpango nae tena kagere kwanza umri ushaenda wamesajiri wachezaji wengi sana zamu yake hishaisha kagere hatasugua benchi sana

    Jibu

    Kwetu rahaaa tuu

    Jibu

    Atakama kwenye Game hiyo kagere Kama atokuwepo kichapo kitawausu tuuu wafanye wafanyavyo simba kiboko yao subilini majabu iyo siku taree 7

    Jibu

    Tuko poa Hata bila Kagere

    Jibu

    Hongera kwao

    Jibu

    N pig kubwa tareh 7

    Jibu

    Namkubali sana kagere

    Jibu

    Kagere jeshi

    Jibu

    Hata hvyo kikosi cha simba kipo vizuri kina masteka kibao walisajiliwa msimu huu

    Jibu

    Kagere yupo gud

    Jibu

    Asnt kwa taarif

    Jibu

    kwetu vicheko tu

    Jibu

    Get well soon Kagere

    Jibu

    Kagere fundi

    Jibu

    Habari mbaya kwa wanamsimbazi kumkosa Kagere kwenye derby

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.