Martinez Katika Hali ya Sintofahamu Inter

Lautaro Martinez anaendelea kuwaumiza vichwa viongozi na mashabiki wa Inter Millan kutokana na kauli yake, “ninafuraha Inter lakini sijajua nini kitatokea kesho” hii ni kauli inayotahadharisha uwepo wake Inter kwa muda mrefu.

Martinez amehusishwa na usajili mkubwa wa kujiunga na miamba ya LaLiga – Barcelona na dirisha la usajili lilimalizika pengine tungeona hilo likitokea lakini haikuwa hivyo.

Akiwa na umri wa miaka 23 pekee, mpaka sasa katika michezo 5 ya Serie A ameshafunga magoli 3 na hakupendezwa na kitendo cha kutolewa katika kipindi cha pili kwenye mchezo dhidi ya Genoa.

Akizungumza kuelekea mchezo wa Ligi ya Mabingwa dhidi ya Shakhtar Donetsk, Martinez amesema, “Ninafanya kazi kubwa kila siku kujiimarisha zaidi. Ninataka kujitoa kikamilifu kwa Inter na wachezaji wenzangu.

“Ninafuraha kuwa Inter. Tunajitahidi kufanya kila tuliwezalo ili tupate mataji na kuirudisha Inter inapotakiwa kuwa.

“Hiki ndicho ninachokiwaza leo. Sijui kitakacho tokea kesho lakini leo ninapenda kuwaambia kuwa ninafuraha kuwa Inter.

“Ninawashukuru mashabiki kwa upendo wanaonionesha na pia kwa wafanyakazi wote wa Inter. Hili ndio jambo muhimu kwangu.”

Inter hawajawahi kupoteza mchezo dhidi ya timu za Ukraine na mchezo wao wa mwisho dhidi ya  Shakhtar Donetsk, Inter walishinda 5-0 katika nusu fainali ya Europa msimu uliopita.


Tsh.160,000,000 Kushindaniwa!

Tunazungumzia mkwanja wa Tshs.160,000,000! Kupitia Kasino ya Mtandaonii ya Meridianbet unaweza kuwa milionea wakati wowote.

Kamata Mkwanja wako HAPA🤑

14 Komentara

    Uongozi hautokubari haondoke inter mda ukifika

    Jibu

    Vizuri martinez

    Jibu

    Martinez usiondoke jamani mashabiki wa inter tumekuzoea

    Jibu

    Martinez bado inter inakuhitaji

    Jibu

    Hapo martizen Kama Barcelona Kama watapeleka ofa kubwa ya kushawish uongozi na martinez mshahara wakutosha natumain wanawez kumuuza martinez lautaro hapo kazi kwa Barcelona kupelek dau la kuelew kwa kinda huyo

    Jibu

    Dah

    Jibu

    Martinez ana mshawasha na barca kwakua yupo mchezaj anaemuhsudu mess ambae yupo nae argentina

    Jibu

    Baki hapo hapo panakufaa.

    Jibu

    Vizuri sana martizen

    Jibu

    Martizen bado inter wanakuitaji

    Jibu

    Abakie hapo mbona panamfaa sana

    Jibu

    Bora asepe tu

    Jibu

    Deal kubwa lipo mbele yake hii ipo wazi lazima atachangamkia fursa ya Barca

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.