Kingsley Coman anataka Bayern Munich kushinda tena mataji matatu (treble) ndani ya msimu mmoja kama walivyofanya msimu uliyopita lakini safari hii anatamani mashabiki kuwepo watakapo pata mafanikio hayo.
Maambukizi ya virusi vya Corona yalisababisha mashabiki ulimwenguni kote kutohudhuria katika viwanja vya michezo mara baada ya soka kurejea, wakati Bayern Munich walifanikiwa kushinda mataji matatu Bundesliga, DFB-Pokal na Champions League bila uwepo wa mashabiki.
Coman alifunga goli pekee na la ushindi katika fainali ya Champions League dhidi ya Paris Saint-Germain mwezi Agosti na kufanya miamba hiyo ya Bavaria kuwa timu ya kwanza katika historia ya mashindano hayo kushinda taji kwa kushinda mechi zote.
Bayern waliendeleza rekodi yao ya ushindi kwa kuifunga Atletico Madrid 4-0 katika kundi A kwa mchezo wa ufunguzi, na mchezo ujao ni dhidi ya Lokomotiv Moscow siku ya Jumanne.
Mashabiki wameruhusiwa kuhudhuria viwanjani nchini Ujerumani msimu huu na Coman anatumaini watashuhudia Bayern ikinyanyua mataji matatu tena msimu 2020-21.
“Yah ni kweli tunataka tushinde treble kila mwaka, tumefanya hivyo msimu uliyopita, bahati mbaya ilikuwa bila mashabiki,” Coman aliiambia CBS Sports.
“Huenda wakaruhusiwa tena mwaka ujao tunataka kufanya kama tulivyofanya tena mbele ya mashabiki zetu.
Coman alifunga mara mbili kwenye mechi dhidi ya Atletico Madrid na kuchangia kuuanza msimu mpya wa Champions League kwa ushindi.
Tunazungumzia mkwanja wa Tshs.160,000,000! Kupitia Kasino ya Mtandaonii ya Meridianbet unaweza kuwa milionea wakati wowote.
aisha
Coman anachosema yuko sahihi kabisa
Sabrina
Duuh hatari sana Coman ameliona hilo
Povel
Coman kingsley yupo sahihi lakin kipind hch cha janga la corona ni vigumu sana kuona mashabik wakiingiah uwanjan ila tuwape muda janga liondoke ili hali irud Kama mwanzo iliwawez kurud mashabik viwanjan
Hopemwaikuka
Coman yuko vzur kinyama
Issa
Kwa moto alionao huyu treble kwa mara ingine
Dorophina
Coman anakiu ya ushindi mbele ya mashabiki lakini ndo haiwezekani kwa kipindi hiki cha corona
Sauda
Mashabiki hawatoweza kuhudhuria uwanjani kipindi cha Corona
Fatina mfingi
Duuh corona inatisha sanaa
Mwajumah
Coman yupo vizuri sana
Lydia Emmanuel Magoti
Coman yupo sahii
Tatu
Coman yupo vizuri
Ester jackson
vigumu sana kuona mashabik wakiingiah uwanjan ila tuwape muda janga liondoke ili hali irudi Kama mwanzo iliwawez kurud mashabik viwanjani
Elika
Yuko sahihi kwa kile alichokisema
warda
Kila kitu mipango tu
Ernest
Bayern wanaweza kupata changamoto kubwa sana kutoka kwa timu nyingine lakini bado wananafasi ya kufanya makubwa tena