Klabu ya Juventus inasubiri majibu baada ya vipimo kwa mshambuliaji Christiano Ronaldo kuangalia kama anaweza kucheza dhidi ya Barcelona katika mashindano ya Champions League.
Ronaldo amewekwa katika matazamio tangu ajulikane kuwa na maambukizi ya COVID-19 wakati wa michezo ya kimataifa akiwa na timu yake ya Portugal mwezi huu, na ameikosa michezo kadhaa dhidi ya Crotone na Hellas Verona katika Serie A pia alikosa mchezo wa UEFA dhidi ya Dynamo Kiev.
Maamuzi kuhusu kupatikana katika mchezo ujao wa Champions League dhidi ya Barcelona ambako kuna mpinzani wake wa muda mrefu Lionel Messisiku ya Jumatano yatatolewa hivi karibuni.
“Amefanya vipimo siku ya leo Jumanne kama watu wote, tunapaswa kusubiri majibu ya vipimo, nadhani yataletwa jioni,” kocha wa Juve Andrea Pirlo alisema.
“Tunatakiwa tusubiri majibu kisha tutaangalia kama atacheza kila kitu bado hakijulikani tuna tumaini tutamuangalia kama atakuwa vizuri kwaajili ya mchezo.
Pirlo pia alizungumzia kuhusu eneo la ulinzi ambalo lina watu kama Giorgio Chiellini na Matthijs de Ligt hawatokuwepo na Leonardo Bonucci ambaye anakabiliwa na kutokuwa fit.
“Kesho tutaangalia wachezaji gani watakao weza kucheza Barcelona ni timu imara tutatakiwa kucheza mchezo mzuri.
“Wachezaji watatakiwa kujitoa sana wenyewe na kucheza kwa bidii.Weston McKennie anafanya mazoezi lakini sidhani kama ataweza kucheza eneo la ulinzi dhidi ya Barcelona.
Tunazungumzia mkwanja wa Tshs.160,000,000! Kupitia Kasino ya Mtandaonii ya Meridianbet unaweza kuwa milionea wakati wowote.
Issa
Covid 19 ni tatizo kubwa inapaswa vilabu vichukue tahadhari kuepuka maambukizi zaid
Hopemwaikuka
Mungu atamjalia atakua salama
Povel
Hapo naona juventus wanajaribu Kama kulazimisha cr7 kucheza kwny mchezo huo muhimu lakin mm naona juventus wangejaribu kumuweka cr7 penden hatakama hatakuwa na negative covid 19 ilikumpa muda wa kupumzika zaid na kufany mazoez kulik kuforce kucheza kwny mtanange wababe kutok catalunya asubir tu
Dorophina
Mungu amsaidie awepo kwenye mechi dhidi ya barca maana yeye ndio msaada mkubwa pale juve
aisha
Duuh corona ni tatizo sana ila atapona pia atarejea kazini kwake
Sauda
Corona ishindwe kwa Ronaldo..
Fatina mfigi
Corona sio powah
Mwajumah
Daaah corona hii ni tishio sana
Lydia Emmanuel Magoti
Duu sio poa gonjwa atari Sana hili
Tatu
Corona imehalibu mipango yake Ronald
Sabrina
Mungu amsaidie apone huu ugonjwa sio poa
warda
Jamani CR7 Nae kapata huu ugojwa sio poa