Chama Aweka Wazi Atakapokwenda

Clatous Chama, nyota wa Klabu ya Simba ameweka bayana mpango wake wa sasa ni kuitumikia timu hiyo na hana mpango wa kuibukia ndani ya Yanga.

Hivi karibuni habari zimekuwa zikieleza kuwa Yanga ipo kwenye mpango wa kuinasa saini ya nyota huyo raia wa Zambia ambaye ana tuzo ya mchezaji bora kwa msimu wa 2019/20 baada ya kutoa jumla ya pasi 10 na kufunga mabao mawili kati ya 78 yalifungwa na Simba.

Kwa sasa Chama mwenye pasi tano na mabao mawili kati ya 22 yaliyofungwa na Simba yupo zake nchini Zambia na timu ya Taifa ambayo jana Novemba 12 ilishinda mabao 2-1 dhidi ya Botswana kwenye mchezo wa kufuzu Afcon.

Chama amesema:”Mimi ni mchezaji wa Simba kwa sasa sina mpango wa kwenda Yanga mjomba, bado nitakuwa ndani ya Simba ikitokea kutakuwa na mabadiliko yoyote kila kitu kitakuwa wazi,” .

Desemba 15 dirisha dogo la usajili linatarajiwa kufunguliwa Bongo ambapo jina ambalo limekuwa gumzo kwa sasa ni nyota huyo ambaye wengi hupenda kumuita mwamba wa Lusaka.

Habari kutoka ndani ya Simba zinaeleza kuwa tayari wamemuongezea mkataba wa miaka miwili utakaomfanya abaki ndani ya timu hiyo yenye ngome yake Msimbazi.


UMEJARIBU HII POKER YA VIDEO?

Jaribu sasa hapa Meridianbet. Ukiacha ukweli kuwa itakupa burudani maridadi, bado inakuhakikishia ushindi mkubwa. Kazi kwako kukusanya ushindi!

Meridianbet Casino

INGIA MCHEZONI!

21 Komentara

    Chama anawez kujiunga na wababe wa jangwan itakua poa

    Jibu

    Atakavyo yy ndo hvyo hvyo

    Jibu

    Chaka abaki tu simba

    Jibu

    Baki tu chama

    Jibu

    wachezaji siku zote wanaangalia maslai tu sio watu wakuwasikiliza sana chama mwili wake huoi simba moyo wake hupo yanga

    Jibu

    Yanga panamfaa sana

    Jibu

    Sisi Yanga tupo full.hatutaki wageni

    Jibu

    Abaki tu simba

    Jibu

    chama abaki tu simba yanga ataenda kufa njaa

    Jibu

    Bora abaki simba

    Jibu

    Abali tu simba

    Jibu

    Chama kubaki simba ni yeye mwenyewe mwenye mamuzi abaki au asibaki ila chama kutoka simba sio laisi yeye ndio amezilisha kuwa Mimi Bado nipo msimbazi mengine hayo maneno yawatu tumeyazoea

    Jibu

    Kwa kauli yake apo ndo kakata mzizi wa fitina maana maneno yalikuwa ni mengi mno

    Jibu

    Yanga awana uwezo wa kumchukua chama

    Jibu

    Bongo wamekuwah hawaelewek wanawez kubadili badilika muda wowote

    Jibu

    Clatious cham mwamba wa lusaka anaweza kaz yake

    Jibu

    Tunaomba liwe kweli karibu sana chamani

    Jibu

    Bongo wamekuwah hawaelewek wanawez kubadili badilika muda wowote

    Jibu

    Abaki tu simbaa

    Jibu

    Chama na simba dam dam

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.