Ulimwengu wa soka na mashabiki wa Real Madrid kwa upekee wao, wanautambua uwezo wa Luka Modric katika safu ya kiungo.
Mkataba wa Luka Modric unamalizika mwishoni mwa msimu huu na hakuna dalili kama anaweza kuongezewa mkataba mpya mpaka sasa.
Licha ya kutokuwa na dalili za mkataba mpya, Modric amefunguka kuwa anataka kuendelea kuwepo Madrid na ameenda mbali zaidi kwa kuongeza kuwa atakuwa mwenye furaha zaidi kama atapata nafasi ya kustaafu maisha ya soka akiwa Santiago Bernabeu.
Akizungumza na waandishi wa habari kuelekea mchezo wa Ligi ya Mabingwa dhidi ya Inter Milan leo usiku, Luka Modric amesema ” Nimesema hili (kwamba ninataka kubaki Real Madrid) mara nyingi lakini tusubiri tuone nini kitakachotokea. Kila mara ninatoa jibu lilelile, ninajisikia vizuri na ninataka kuendelea kuwepo Madrid.

“Ninahisi ninaweza kuisaidia timu, kama utaniuliza ni nini ninahitaji, ninahitaji kubaki. Ninataka kumaliza maisha ya soka nikiwa hapa lakini hilo litategemea mambo mengi. Hakuna mtu atakuwa mwenye furaha kunizidi mimi kama nitastaafia hapa.
“Ninajisikia vizuri. Michezo ambayo sikucheza ni kutokana na maamuzi ya kocha na ninapocheza, ninajaribu kufanya vizuri.
“Wanaongelea sana hali yangu lakini tusubiri tuone ni nini kitatokea mbeleni.”
Je, Real Madrid watachukua uamuzi wa kumbakiza Luka Modric klabuni hapo au wataamua kuachana naye mkataba wake utakapo malizika? Madrid wameanza vibaya Ligi ya Mabingwa msimu huu wakiwa wameshinda mchezo 1 kati ya 3. Ushindi dhidi ya Inter leo usiku utawapa matumaini ya kuendelea kusalia kwenye Mashindano ya msimu huu.
Hadi 130,000,000 TSH Kutolewa kwa washiriki wa shindano la Playson Cashfall. Unaipata kwenye Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet Pekee. Jisajili sasa, kisha ingia mchezoni kabla ya Novemba 29.



Adelta
Inawezekana kwa sababu ni mchezaji mzuri wa Real madrid
magdalena
kaona madrid ndo panamfaa kustaafia
Mwajumah
Kama anaona panamfaa kustaafu akiwa apo ni vizuri zaidi kwan uamuzi ni wake yeye
Caroline
Modrick Madrid ungeendelea kukaa apo kwa kua.ndio timu yako pendwa
Sania
Ndio patamfaa
Sauda
Inawezekana kabisa.
Rahma
Nice
Ester jackson
Uwamuzi ni wake kama patamfaa
Nasra
Safii
Khadija
Maamuzi ni yakwake kama panamfaa hau laah!
Fatina mfingi
Nice
Hopemwaikuka
Sio mbaya ukibak hapo hapo
aisha
Katika dunia hakuna kinachoshindikana
Angelina
Kila kitu kinawezekana
Povel
Hapo ni maamuzi yake kuendeleah kucheza ndani ya madrid mpaka hatakapo fikiah final kucheza soka
Saupha mohamed
Panamfaa sana tyuu
Dorophina
Modric ameona madrid ndio sehemu sahihi kwake kuitumikia mpaka atakapofikia hatua ya kustaafu
Sadick
Kiwango Modric kimeshuka na Madrid inatakiwa kusajiri wachezaji wenye viwango kuendelea kubaki ktk ubora na Kocha anamuona hana msaada tena ndio maana anamuweka bench
Issa
Modric kustaafu madrid inawezekan ila kwa mchezaj kama huyu ambae historia inambeba atahitaj kuondokaa kuweka rekod timu zingin
Gabriel
maamuzi yake kuendelea kucheza ndani ya madrid
neema hassan
Asante kwa makala
samiah
Gud
Latifa juma mohamed
Hakuna kinachoshindikan
Tatu
Panamfaa sana tu
Lydia Emmanuel Magoti
Modric akaona Pana mfaa apo ndomana anataka kustarfu apo
Sarah
Nice
warda
Wamuongezee tu jamani