Dominic Szoboszlai Atua RB Leipzig.

Baada ya kuhusishwa na vilabu kadha wa kadha, hatimaye Dominic Szoboszlai ameichagua RB Leipzig na sasa anatimkia Bundesliga.

Arsenal, AC Millan na Real Madrid ni miongoni mwa vilabu vilivyohusishwa zaidi na sahihi ya Szoboszlai ambaye anakipiga katika klabu ya RB Salzburg.

Hii ni habari mbaya zaidi kwa Arsenal ambao walimtizama Dominic Szoboszlai kama mbadala sahihi wa Houssem Aouar ambaye walimkosa majira ya kiangazi.

Szoboszlai baada ya kukamilisha usajili wa RB Leipzig

RB Leipzig wameipata sahihi ya Szoboszlai kwa kulipa pauni milioni 18 ikiwa ni dau tofauti na ambalo vilabu vingine vilitakiwa kulipa (pauni milioni 23).

Kwa Mikel Arteta hili ni pigo kutokana na uhalisia kwamba timu yake haina mchezaji mwenye haiba ya Szoboszlai kwa sasa na wanapata tabu sana katika safu yao ya kiungo mchezeshaji. Ni Mesut Ozil pekee mwenye uwezo wa kutibu tatizo hilo lakini hayupo kwenye mipango ya kocha huyo msimu huu.


BURUDIKA NA WANYAMAPORI WAKIIMBA NA KUPIGA VYOMBO VYA MUZIKI!

Kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, furahia mchezo wa Forest Rock. Hapa utaburudika na umahiri wa wanyapori wanaoimba na kutumia vifaa vya muziki wa rock. Burudika huku ukijiwekea nafasi ya kutengeneza pesa ndefu kupitia Meridianbet!!

INGIA MCHEZONI!

12 Komentara

    Hii ni habari mbaya kwa kikosi Cha Arsenal

    Jibu

    Kapambane tu

    Jibu

    Habari njema

    Jibu

    Duu

    Jibu

    Habari njema kwa mashabiki wa rb leipzig

    Jibu

    Rb imepata mtu

    Jibu

    Safi

    Jibu

    Safiii sana

    Jibu

    Good

    Jibu

    hongera yake

    Jibu

    Popote kambi

    Jibu

    Kambi popote

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.