Hakuna Mazungumzo ya Mkataba wa Dembele

Winga wa Bercelona, Ousmane Dembele amethibitisha kuwa hakuna taarifa yeyote ya ziada juu ya mazungumzo ya kukubaliana mkataba mpya na Barcelona.

Ronald Koeman amekuwa akisisitiza nia yake ya kutaka kumbakiza nyota huyu wa Ufaransa pale Camp Nou wakati mkataba wake wa sasa ukiwa unafika mwisho mwisho wa msimu ujao.

Hata hivyo, hakujawa na maendeleo yeyote kwenye mazungumzo ya mkataba mpya, kwa mujibu wa Dembele kama alivyonukuliwa na Marca. Licha ya kuwepo na hali hii Dembele bado ana matumaini kuwa hatma yake klabuni hapo itapewa umuhimu.

“Hakuna mazungumzo yeyote bado juu ya mkataba mpya, lakini najihisi vyema tu” – Ousmane Dembele

Ousmane Dembele

Nyota huyu wa zamani wa Borussia Dortmund anafurahia msimu wake bomba akiwa na Barcelona, akiwa sehemu ya ushambuliaji pamoja na Lionel Messi, Antoine Griezmann.

Nyota huyu wa miaka 23 amebainisha kuwa kwa mwaka 2021 amefurahia zaidi kucheza kama mshambuliaji, na amecheza jumla ya mechi 24 za ligi kwa msimu huu wa 2020-21.


 

JILIPE KWA NAMBA ZAKO ZA BAHATI NA KENO

Kila mtu ana namba zake za bahati, Meridianbet tunatambua namba zinaweza kukufanya milionea leo. Jilipe kwa namba zako za bahati kila baada ya dakika tano.

CHEZA HAPA

 

5 Komentara

    Dembele ni bora abakie camp nou

    Jibu

    Dembele yuko vizuri

    Jibu

    Dembele yuko vinzur

    Jibu

    Eeh

    Jibu

    Hawawezi muuza mpaka wapate mbadala

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.