PSG: Hakuna Mpango wa Kumuuza Mbappe

PSG hawapo tayari kumuachia Kylian Mbappe. Tetesi za usajili za Real Madrid zimekuwa zikimtazama na kumuhusisha Mbappe na klabu hiyo.

Lakini, taarifa zinasema kuwa mipango ya uhamisho ya Real Madrid kwenye msimu ujao wa joto kwa kiasi kikubwa imekuwa ikiathiriwa na mpango wa PSG kusalia na Kylian Mbappe.

Real walikuwa wanahusishwa na uhamisho wa gharama wa nyota huyu tangia dirisha la usajili lililopita. Taarifa za uhamisho wa Mbappe zimekuwa na sura ya tofauti mtaani hivi karibuni baada ya kuonekana kuna kusuasua katika makubaliano ya mkataba mpya.

Kylian Mbappe PSG

Mbappe kwa sasa amesalia na miezi 12 kwenye mkataba wake pale Parc de Princes, huku PSG bado wakiwa mbali na maafikiano ya kusaini mkataba mpya, hali inayopelekea kuwepo na minong’ono mingi juu ya hatma yake.

Hata hivyo, licha ya sintofahamu ya hatma ya staa huyu, raisi wa PSG Nasser Al-Khelaifi amethibitisha kuwa klabu inafanya kila iwezalo kumbakiza staa huyu.

“Ninahitaji kuweka sawa. Mbappe atasalia Paris, kamwe hatutamuuza, na kamwe hataondoka bure.” Nasser Al-Khelaifi


WEKA PESA KUPITIA DUKANI MERIDIANBET!

Chukua namba yako ya akaunti na kiasi cha pesa unachotaka kuweka, sogea kwenye duka lolote la Meridianbet lililo karibu nawe utasaidiwa kuweka pesa.

Weka Pesa Meridianbet

WEKA PESA

4 Komentara

    Bora mbappe abaki apo apo

    Jibu

    Itakuwa poa sana mbappe akibakia

    Jibu

    Bora mbappe akibakia PSG

    Jibu

    Mbappe abaki tu

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.