Baada ya kuingia kwenye hatua ya robo fainali, watu wengi waliibeza sana lakini ni rasmi sasa Kaizer Chiefs wametinga hatua ya fainali ya kombe la klabu bingwa Afrika baada ya kuingia katika michuano hiyo kwa mara ya kwanza.
Kaizer Chiefs ambao walikuwa wakicheza na Waydad Casablanca jana usiku katika mechi ya marudiano walifanikiwa kutoka sare ila goli moja walilopata katika mechi ya mkondo wa kwanza kule Morocco ikawabeba na sasa wapo fainali.
Mechi ya mkondo wapili iliyopigwa jana ilishuhudia Kaizer wakicheza kwa tahadhari sana huku wakishambulia kwa nafasi na mpaka dakika tisini zinakamilika, Kaizer 0, Waydad Casablanca 0.
Hivi sasa Kaizer Chiefs watakutana na mabingwa watetezi wa Kombe hilo Al Ahly ambao nao wametinga hatua ya fainali baada ya hapo jana kumpiga Esperance ya Tunisia 3-0, na kuwa magoli ya ujumla ya 4-0.
Mashabiki na wadau wengi wa soka Tanzania wanaamini kwamba nafasi aliyo the Amakhos kwa sasa ilitakiwa kuwa ya Simba endapo wangekuwa na bahati kidogo tu, lakini kiukweli ni kwamba Simba hawakujitoa sana katika mechi ya robo fainali ya mkondo wa kwanza.


