Tetesi zinasema, Paris St-Germain wanataka dau la £188m kutoka Real Madrid kwa ajili ya mshambuliaji wake Mfaransa Kylian Mbappe, 22.
Manchester City wanaweza kumgeukia mshambuliaji wa Juventus na Ureno Ronaldo, 36, baada ya nahodha wa England, Harry Kane kusema anabaki Tottenham.
Tetesi zinasema, Meneja Pep Guardiola ataondoka Manchester City pale mkataba wake utakapomalizika msimu wa mwaka 2022-23 ili kupumzika kabla ya kuhamia kufundisha timu za taifa.

Tetesi zinasema, Meneja wa Arsenal Mikel Arteta hawezi kufukuzwa licha ya washika bunduki hao kuanza vibaya msimu huu wa ligi kuu ya England.
Meneja wa Roma Jose Mourinho amepanga kutumia £13.5m kwa ajili ya kiungo wa Chelsea muingereza Ruben Loftus-Cheek, 25. Nyota huyo aliwahi kufanya kazi na Mourinho wakati mreno huyo aliporejea kuifundisha Chelsea kwa mara ya pili.
Manchester United haitaweza kupeleka dau kwa ajili ya kiungo wa Rennes mfaransa Eduardo Camavinga, 18, au kiungo wa Atletico Madrid na Hispania Saul Niguez, 26, kama haitauza wachezaji wake kupata fedha za kuingia sokoni.
Tetesi zinasema, Sevilla wanasema walikataa ofa ya Chelsea kwa ajili ya mlinzi wake mfaransa Jules Kounde,22 na hawahitaji kuuza wachezaji.

Kiungo wa Barcelona Ilaix Moriba huenda akatua Chelsea ama RB Leipzig kama kinda huyo mwenye umri wa miaka 18 raia wa Guinea hataongeza mkataba mpya na vigogo hao wa Laliga.
Tetesi zinasema, Winga wa Arsenal na Brazil Willian, 33, anajaribu kukamilisha uhamisho wake kuelekea Corinthians.
Koungo wa zamani wa Arsenal na England Jack Wilshere, 29, anafikiria kustaafu soka baada ya kukosa ofa ya kujiunga na klabu yoyote tangu aachwe na klabu ya Bournemouth.
Kiungo wa Barcelona na Hispania Sergio Busquets amekubali kukatwa tena mshahara wake ili kusaidia wakali hao wa Laliga kupunguza mzigo wa mishahara klabuni.
Unawezaje kuikosa hii! Ndani ya kasino za meridianbet kuna mchezo unaoweza kukupa mkwanja mrefu leo hii, Wild Hot 40 ni njia nyingine ya kukufanya milionea, Chagua namba yako na uvune mkwanja.



Sarah
Ziko bomba
Issa
Saf