Wiki ya 12 kunako Premier League hii hapa moja ya mechi za kuvutia siku ya leo Jumamosi ni hii kati ya Liverpool dhidi ya Arsenal mechi itapigwa katika dimba la Anfield.

Liverpool wapo mbele ya Washika mitutu wa London kwa tofauti ya alama 2 pekee hivyo Liver wenye alama 22 watalazimika kushinda mchezo huu ilikupunguza presha.
Wachezaji wa Liverpool Sadio Mane, Andrew Robertson na Jordan Henderson wote wanasumbuliwa na majeraha waliyopata wakati wa majukumu na timu za taifa.
Lakini Klopp amethibitisha kwamba Mane atacheza dhidi ya Arsenal vilevile Robertson anatarajia kuwa sehemu ya mchezo huo.
Divock Origi alipata jeraha la kichwa wakati akiwa na timu ya taifa ya Ubeligiji lakini anatarajia kukichafua dhidi ya vijana wa Arteta.
Kwa Upande wa Arsenal Thomas Partey atakuwa fit, Folarin Balogun pia anatarajia kuwa kwenye kikosi cha Gunners lakini Granit Xhaka na Sead Kolasinac watakosa mechi hii.
Arteta huenda akawatumia washambuliaji wake Alexandre Lacazette na Pierre-Emerick Aubameyang wakati ni kama Pepe, Bernd Leno, Martin Odegaard na Gabriel Martinelli watakuwa katika benchi.
Kikosi cha Liverpool Kinachoweza Kuanza: Alisson; Alexander-Arnold, Matip, Van Dijk, Robertson; Oxlade-Chamberlain, Fabinho, Thiago; Salah, Jota, Mane
Kikosi cha Arsenal Kinachoweza Kuanza: Ramsdale; Tomiyasu, White, Gabriel, Tierney; Saka, Thomas, Lokonga, Smith Rowe; Lacazette; Aubameyang
Unasababu milioni za kucheza unavyotaka ukiwa na mabingwa meridianbet, lakini unasababu moja ya kushinda mamilioni katika kasino za mtandaoni za meridianbet. Mchezo maridhawa wa Crazy Time unakupa sababu hizo kuwa mmoja wa washindi leo hii.


