Michael Carrick, msimamizi wa klabu ya Manchester United ataendelea kuwa kwenye benchi na kuingoza timu Man Utd dhidi ya Arsenal siku ya alhamisi kwenye mchezo wa ligi kuu ya Uingereza licha ya kupatikana kocha wa muda.
Man Utd walimtangaza Ralf Rangnick kama kocha wa muda mpaka mwisho wa msimu siku ya jumatatu lakini hataweza kuwa kwenye benchi kwa sababu ya maswala ya vibali kutokukamilika.

Rangnick mwenye umri wa miaka 63 amejiunga na Man Utd akitokea Lokomotiv Moscow, ambako alikuwa meneja maendeleao ya michezo na anatarajiwa kuchukua mikoba ya kuinoa Man Utd mpaka mwisho wa msimu, na baadae kuwa mshauri kwa miaka miaka miwili.
Kufuatiwa na mechi dhidi ya Arsenal siku ya alhamisi, pia jumapili Man Utd watakuwa na kibarua kizito cha kuwakaribisha Crystal Palace wenye dimba la old trafford, baada ya hapo wataenda cheza na timu kutoka Uswiss, Young Boys kwenye ligi ya mabingwa tarehe 8 disemba mchezo ambao unaweza kuchezwa kwenye “neutral venue” kutokana na corona.
Mabingwa Meridianbet hawajawahi kukuacha mnyonge hasa katika kipindi hiki cha msimu wa sikukuu, kasino maridhawa ya Carnaval Jackpot inakupa thamani ya dau lako. Kuwa mmoja wa washindi leo hii.


