Ryan Garcia alijitokeza Jumamosi iliyopita usiku kwenye mitandao ya kijamii akisema anataka kurejea ulingoni na anamtka George Kambosos Jr baada ya kumtazama akimchapa Teofimo Lopez.

Baada ya kuwakatisha tamaa mashabiki mwaka mzima, Ryan (21-0, 18 KOs) alisema kwa ujasiri kwamba atapambana na bingwa asiyepingika wa uzani wa lightweight Kambosos kurejea ulingoni. Ryan anafikiria nini?
“Pambano langu la kurudi, nitapigana na Kambosos’ Ryan Garcia alisema kwenye Twitter.
Sean Jones ana shaka kuwa wakati huu itamfaa Ryan. Nadhani Ryan hatimaye amepata bingwa ambaye hatakubali kumpa ushindi kirahisi, hasa baada ya kushuhudia upiganaji wake mbaya abanapokuwa ulingoni.
Kambosos (20-0, KO 10) aliweka wazi hilo siku ya Jumamosi iliyopita usiku baada ya kumchapa Teofimo kwa kusema kwamba anataka kupigana na bondia aliye bora zaidi.
Mabingwa Meridianbet hawajawahi kukuacha mnyonge hasa katika kipindi hiki cha msimu wa sikukuu, kasino maridhawa ya Carnaval Jackpot inakupa thamani ya dau lako. Kuwa mmoja wa washindi leo hii.


