Barcelona walifungwa bao la dakika za lala salama siku ya Jumamosi dhidi ya Real Betis mchezo uliyoisha kwa ushindi wa 1-0 kwenye LaLiga na kufanya kocha Xavi Hernandez kupoteza mchezo wa kwanza tangu alipopewa jukumu la kuwa kocha mkuu wa Barca.

Ulikuwa ushindi wa kwanza kwa Betis wakiwa dhidi ya Barca zaidi ya miaka mitatu na kuwapeleka hadi nafasi ya tatu wakiwa na pointi 30, pointi sita nyuma ya viongozi Real Madrid ambao baadaye walipata ushindi wa 2-0 dhidi ya Real Sociedad. Barcelona wako katika nafasi ya saba kwa alama 23.
Huku mechi ya mwisho ya Barca ikiwa ugenini dhidi ya Bayern Munich itakuwa siku ya Jumatano, Xavi aliwapumzisha wachezaji wake watatu muhimu – Gerard Pique, Frenkie de Jong na Ousmane Dembele.

“Tulipokuwa kwenye ubora wetu, bao lilipatikana kwenye shambulizi la kushtukiza,” alisema Xavi.
“Tulijua mabadiliko yao, tulikuwa na dakika chache nzuri, ni adhabu kali sana kwa mchezo tuliocheza, ni kipigo kinachoumiza, nyumbani tulikuwa kwenye hali nzuri, lakini ndivyo soka lilivyo.
Mabingwa Meridianbet hawajawahi kukuacha mnyonge hasa katika kipindi hiki cha msimu wa sikukuu, kasino maridhawa ya Carnaval Jackpot inakupa thamani ya dau lako. Kuwa mmoja wa washindi leo hii.


