Erik Ten Hag amekuwa akihusishwa na kuahamia kwenye klabu ya Manchester United kuchukua mikoba iliyoachwa na Ole Gunnar Solskjaer baada ya kufungashiwa vilago kutokana na kuwa na muendelezo mbaya, pia Erik Ten Hag amekubali kuwa yuko tayari kwa changamoto mpya nje ya Ajax
Man Utd walimfuta kazi Ole Gunnar Solskjaer mwezi uliosha na kocha wa Ajax Erik alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa wanapewa nafasi kubwa ya kurithi mikoba hiyo ingawa Man Utd walimteuwa Ralf Rangnick kuwa kocha wa muda mpaka mwisho wa msimu.

“Nahisi niko tayari kwa hili, na nitakuwa na furaha kupata changamoto mpya, lakini siifukuzii, kama ikishindikana, siwezi sema kuwa kazi yangu ya ukocha ndio imefeli.” Erik Ten Hag alipoulizwa kuhusu uvumi wa yeye kuitaka Man Utd.
Erik Ten Hag amezaliwa mwaka 1970 pia alikuwa mchezaji wa Uholanzi na kwa sasa anaifundisha klabu ya Ajax ambayo ameiwezesha kuchukua ubingwa wa ligi kuu ya Uholanzi na vile vile kuwafikisha hatua ya nusu fainali ya ligi ya mabingwa Ulaya mwaka 2019.
| Timu alizofundisha | |||
|---|---|---|---|
| 2012–2013 | Go Ahead Eagles | ||
| 2013–2015 | Bayern Munich II | ||
| 2015–2017 | Utrecht | ||
| 2017– | AFC Ajax | ||
Mabingwa Meridianbet hawajawahi kukuacha mnyonge hasa katika kipindi hiki cha msimu wa sikukuu, kasino maridhawa ya Carnaval Jackpot inakupa thamani ya dau lako. Kuwa mmoja wa washindi leo hii.


