Gonzalo Higuain amesema kwamba washambuliaji Kylian Mbappe na Erling Haaland ni warithi wa mahasimu wawili waliyotawala soka kwa zaidi ya miaka 10 Lionel Messi na Christaino Ronaldo.

Fowadi huyo wa klabu ya Major League Soccer ambaye alifunga mabao 107 katika mechi 190 wakati akicheza katika LaLiga akiwa na Real Madrid kati ya mwaka 2007 na 2013 anaamini Mbappe akienda Madrid atarejesha klabu hiyo juu kwenye soka la Ulaya.
Wachezaji wote Haaland na Mbappe wamekuwa wakihusishwa kwenda Bernabeu na Mbappe alifungia PSG bao pekee kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa hatuaya 16 bora lakini ripoti za hivi punde zinadai Mbappe anaweza kuukosa mchezo wa marudiano sababu ya jeraha alilopata akiwa mazoezini.
“Mbappe anasifa zote,” Higuain aliiambia Stats Perform. “Naamini Messi na Ronaldo watacha kucheza siku si nyingi sababu maisha yapo kama hivyo na Mbappe na Haaland watafanikiwa kuchukua utawala.

Pia tetesi zinadai Real Madrid na Manchester City ndiyo wanaongoza kwa kuiwania sani ya mshambuliaji hatari Erling Haaland mwenye umri wa miaka 21.
Mchongo mpya mjini ni Shindano la Evoplay Spring Aweking katika kasino maridhawa za meridianbettz. Pata mgao wako wa TSh 25,000,000 katika michezo kibao ya kasino na sloti ziliyochaguliwa kushiriki.


