Staa Zlatan Ibrahimovic amesema kwamba amewasahihisha wenye mashaka na yeye baada ya kudhihirisha umri ni namba tu kufuatia kusaini mkataba mpya huko Milan.
Nyota ya Ibrahimovic imeng’aa tangu alipojiunga tena na Milan kwa uhamisho huru akitokea LA Galaxy mwaka 2019 starika huyo mkongwe amefunga mabao 15 katika michezo 17 ya Serie A msimu huu.
Mshambuliaji huyo wa miaka 39 sasa anamkataba na Rossoneri mpaka mwisho wa msimu 2021-22 na amefunga mabao 17 kwenye mashindano yote wakati pia amefunga mabao 28 katika michezo 45 katika awamu yake ya pili huko Milan.
“Nadhani itakuwa vizuri, hata kama kuna mtu ana mashaka na wewe,” Ibrahimovic aliiambia Milan TV. “Nimeonesha kuwa umri si chochote.
“Ni swala la akili yako, mara nyingi nimekuwa nikitaka kuimarikana kufanya vizuri kadri ya uwezo wangu.
Ibrahimovic aliisaidia Milan kutwaa Scudetto mwaka 2011 msimu wake wa kwanza na ameisadia kukaa katika nafasi ya pili msimu huu nyuma ya mahasimu wao wa jiji kwa tofauti ya alama 10.
Nafasi nyingine kwaajili yako, kasino mpya yenye hadhi ya kipekee inayokupa kila sababu ya kuwa mshindi katika kasino za Meridianbet, anza siku yako na njia rahisi ya kutengeneza mkwanja.
Adelta
Ibrahimovic mambo ni 🔥🔥🔥🔥
aisha
Kazi nzuli namkubali sana
Lydia Emmanuel Magoti
Yupo vizuri movic
Saupha
Yupo vizurii
Magdalena
Kazi nzuri amefany
Khadija
Ibra mtu mbaya
Issa
Kadabra
Elika
Ibra yuko vizuri sana
Johnmary jo
Namkubari sana ni mchezaji mzuri#
Meridianbett #
warda
Huwa namkubali sana