Marseille Kumsaini Saliba Kutoka Arsenal kwa Mkopo

Beki wa Arsenal William Saliba ametua Ufaransa kuelekea Marseille ambako amesajiliwa na klabu hiyo kwa mkopo.

Marseille Kumsaini Saliba Kutoka Arsenal kwa Mkopo

The Gunners walikuwa kwenye mazungumzo na klabu hiyo ya Ligue 1 kwa wiki kadhaa kuhusu dili ya mkopo wa mchezaji huyo wa miaka 21 ambaye alitumia nusu ya msimu na klabu ya Nice kwa mkopo.

Na makubaliano sasa yamefikiwa na mlinzii huyo amepewa ruhusa ya kwenda Ufaransa kukamilisha uhamisho wake huko The Stade Velodrome.

Saliba alitua Ufaransa siku ya Jumanne asubuhi kwaajili ya kufanyiwa vipimo na kukamilisha usajili wake na Marseille.

Hii itakuwa mara ya tatu kuondoka kwa mkopo tangu atue Emirates mwaka 2019 kwa dau la £27m ($37m) akitumie misimu na Saint-Etienne na Nice.

Marseille Kumsaini Saliba Kutoka Arsenal kwa Mkopo

Arsenal wanadai bado wanamipango na beki huyo licha kutolewa kwa mkopo na watamuangalia tena mwisho wan msimu 2021-22.

Arsenal sasa wanaendelea na mipango yao ya kutaka kuinasa saini ya beki wa kati wa Brighton Ben White dili ambayo inasemekana inaweza kufika £50m.


JIUNGE NA FAMILIA YA MABINGWA!

Ndio, kama bado hujajiunga na Familia ya Mabingwa ya Meridianbet, huu ndio wakati wako! Tunakupatia Bonasi ya 3,500 Tsh papo hapo kama sehemu ya ukaribisho!

Italia, Italia Bingwa Euro 2020., Meridianbet

JIUNGE SASA!

 

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.