Dele Alli yuko huru kuondoka Tottenham Hotspur Januari hii, alipoteza nafasi yake katika timu ya Spurs chini ya Jose Mourinho na hakuweza kuondoka kwa mkopo licha ya kuhusishwa na Paris Saint-Germain.

Muda wa Nuno Espirito Santo kuinoa Spurs ulionekana kana kwamba ungemruhusu Dele kurejea katika kiwango chake bora, lakini amerudi nyuma chini ya kocha wa sasa Antonio Conte.
Hapo awali, Spurs walisita kumruhusu kiungo huyo aondoke na Daniel Levy alipambana na Paris Saint-Germain mwaka 2020 na Januari 2021, lakini sasa Fabio Paratici, mkurugenzi mkuu na Conte wote wamekubaliana kwamba milango iko wazi kwa ajili yake.
The Athletic, hata hivyo, wameripoti kuwa vilabu vinasita kufikia dau la Spurs kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25, na mkataba wake ukiendelea hadi 2024.
Chini ya Conte, Dele amecheza mechi moja pekee ya Premier League, ambayo ilikuja kama mbadala katika ushindi wao dhidi ya Leeds United.
Fanya wiki yako iwe ya ushindi mkubwa ndani ya kasino za mtandaoni za meridianbet. Mchezo wa BURST THE BANK🔥🤑 ni moja kati ya mchezo pendwa unaowapa wachezaji mamilioni kila siku. Kwa dau dogo unashinda zaidi.


