Aston Villa wamemchagua Steven Gerrard kama kocha mkuu wa klabu yao kwa dili ya miaka mitatu na nusu.
Aston Villa “Tunafurahi kutangaza kumchagua Steven Gerrard kuwa kocha mkuu wa klabu yetu.
Gerrard alisema “Aston Villa ni klabu yenye utajiri mkubwa na tamaduni wa soka la Uingereza ninajivunia kuwa kocha mkuu wake mpya.
“Ningependa kutoa shukrani zangu za dhati kwa kila mtu anayeshirirkiana na Rangers kwa kunipa fursa ya kuisimamia klabu kubwa ya mpira wa miguu. Ningependa kuwatakia wachezaji, wafanyakazi na mashabiki kila la kheri kwa siku za badaye.
Gerrard ameondoka Scottish Premiership akiwaacha Rangers wakiwa kileleni kwa tofauti ya alama nne safi huku akifanikiwa kuwapa taji hilo baada ya kwenda miaka 10 bila kutwaa taji hilo.
Steven anajulikana kuwa moja ya wachezaji bora kabisa wa Premier League wakati akiichezea Liverpool na sasa anaenda kuonyesha upande ukufunzi kwenye EPL.
Alicheza mechi 710 akiwa na Liverpool akifanikiwa kushinda mataji tisa huku akiwa na kumbukumbu ya kushinda taji la Ligi ya Mabingwa.
Steven Gerrard wakati akichezea Liverpool hakufanikiwa kushinda taji la Premier League, Je ataweza kubeba akiwa kama kocha?
Unawezaje kuikosa hii! njia rahisi ya kutengeneza mkwanja katika kasino maridhawa za meridianbet. Muda wa kufurahia na kutengeneza mkwanja ipo mikononi mwako unasubiri nini?