Thomas Tuchel amekiri kwamba angependa kuwa na Harry Kane kama sehemu ya kikosi chake cha Chelsea, lakini alisema kwa ufupi tu Chelsea inavutiwa na straika huyo.

Kane amekuwa akihusishwa na kusepa zake huko Tottenham na timu kubwa nyingi zimekuwa zikivutiwa na huduma ya mshambuliaji huyo ikiwe na klabu ya Stamford Bidge.
“Kama ukitafuta kocha yoyote ulimwenguni ambaye atamtaka Harry Kane katika timu yake niite tena. Ningependa kuongea na mtu huyo na kusikiliza mawazo yake katika eneo la ushambuliaji na ufungaji,” Tuchel alisema katika mkutano na waandishi wa habari.
“Kila mtu anampenda Harry Kane lakini acha tuwe wawazi tu, ni mchezaji wa Tottenham. Anamktaba wa muda mrefu na hatutojihusisha katika mkutano wowote na waandishi kuhusu hilo tena.”

Ikumbukwe Harry Kane alipeleka ombi la kutaka kuachana na klabu hiyo ya London kwa kile alichodai anataka kushinda mataji.
Zungusha na ushinde mkwanja wako papo hapo baada ya mzunguko kukamilika. Ni kugusa tu 🤑.



Magdalena
Kane yupo vizuri
Sarah
Kane yuko vizuri