FIFA Kuruhusu Wachezaji 26 Kwenye Michuano ya Kombe la Dunia

Shirikisho la mpira wa miguu duniani FIFA limeruhusu wachezaji 26 kutoka wachezaji 23 wa awali, ambapo kuanzia kwenye michuano ya kombe la dunia ya mwaka huu 2022 inayokwenda kuchezwa Qatar kuanzia mwezi Novemba.

Makocha wote wa timu za taifa wataruhusiwa kuwa na wachezji wote 26 kwenye michezo yao ya siku, huku makocha wakiwa na wigo mpana wa kuchagua wachezji 15 kutoka benchi.

FIFA

Kwa mara ya kwanza timu za taifa ziriruhisiwa kuwa na wachezaji 26 badala ya 23 kwenye michuano ya Euro 2020  kwenye majira ya kiangazi yaliopita, kwa sababu ya mlipuko wa Uviko-19. lakini ni wachezaji watatu tu ndio hawakupaswa kuwepo kwenye mchezo wa siku hiyo.

Pia shirikisho la mpira wa miguu duniani FIFA limetoa ukomo wa kuwasilisha majina ya wachezaji ambao watapaswa kuyawakilisha mataifa yao hadi Novemba 13, baada ya hapo hakutakuwa na muda wa ziada wa kuwasilisha majina.

FIFA hivi karibuni pia walitangaza kuongeza idadi ya maingizo ya wachezaji kutoka wachezaji 3 hadi 5 kwenye mchezo wa siku.


ALIYA’S WISHES

Bila shaka unatamani ushindi mkubwa, vipi kuhusu kujaribu Sloti hii ya Aliya’s Wishes? jaribu ushinde sasa.Kasino ya Mtandaoni

CHEZA SASA

Acha ujumbe