Danny Rose anapenda kupata fursa ya kucheza mbele ya mashabiki wa Tottemham kwa mara nyingine na atafurahi kama atamaliza muda uliyobaki katika mkataba wake akiwa na Spurs.
Beki wa kushoto wa England Rose ametumia nusu ya msimu wa 2019-20 katika Premier League kucheza katika klabu ya Newcastle kwa mkopo baada ya kutokuwa chaguo la kocha Jose Mourinho pindi alipochukua nafasi ya Pochettino kuinoa Spurs mwezi Novemba mwaka uliyopita.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 aliiambia BBC Radio 5 Live anajihisi “Hakupewa nafasi kubwa ya kucheza kama watu wengine katika safu ya ulinzi” na kocha Mourinho.
Rose yupo kwenye mkataba na timu ya Tottenham mpaka mwaka 2021 mwezi Juni na aliiambia The Second Captains amekuwa akitamani kufufua matumaini ya kuendelea kucheza katika klabu hiyo.

“Nitafurahi kukaa Tottenham na kuona miezi 10-11 iliyosalia naimalizia hapo,”
“Hakuna chochote ninachokihitaji zaidi ya kucheza nahitaji kucheza mbele ya mashabiki Spurs.
“Mechi yangu ya mwisho kucheza nikiwa na Tottenham ilikuwa ni dhidi ya Liverpool tulipoteza kwa 1-0 sikujua kama ndiyo mchezo wangu ma mwisho klabuni.”
Rose alishawahi kuhusishwa na kuhamia Manchester United, alikuwa ni beki mchezeshaji chini ya kocha Pochettino pia alikuwa ni sehemu ya timu ya England mwaka 2018 walipofika hatua ya nusu fainali katika michuano ya kombe la dunia.
Rose alifunga goli dhidi ya Arsenal mwaka 2010 katika Premier League na ameichezea Spurs michezo 210 katika mashindano yote.
Tiketi yako ya kwanza kamwe haiwezi kupoteza ukiwa na Meridianbet. Unarudishiwa 100% ya Tiketi yako ya kwanza.


Amiri Kayera
Anamapenzi na team
Leonard
Rose mchezaji mzuri
Povel
rose majeruh ndo yamemfany kupotezah namba spur na kupelekea kutolew kwa mkopo Ila natumain atafany vzr atarud Tena kuchez na Uzi wa spur kikubw jitihad na maarifa haongezeh huko alipo thnk meridian bet tz kwa update
Shafii
Kiukweli rose asikiki kabisa saivi majeruhi ya Mara kwa Mara ndilo tatizo kwake.
Theonestina
Asante meridianbet kwa taarifa
Hope mwaikuka
Kama kuna kulipa rud tu
Samiah
Gud news
Sabrina
Arudi tu kama anaona masirahi yapo spurs
farida ahmadi
Harudi tyuu Spurs akakipige
Latifa juma mohamed
New updates.
Aziza mushi
Habari njema.
Venerose
Kama masilah yapo wewe rud
Fatuma kasomo
Arudi tu
Magdalena
Majerui ndo yamemfanya apoteze dira uyu jamaa
Dorophina
Habari njema hii itakuwa poa sana rose akirudi spurs kuichezea klabu yake
aisha
Rose acha kuhangaika unatakiwa utulie sehemu moja ili utengeneze mafanikio yako ya baadae kwasababu mpira unamwisho huwezi kucheza milele
Nasra
Bora rose arudi kwenye timu tu
Ester jackson
Daah rose yupo nishamsahau kabisa kijana mjeuri ambaye anajituma ila wakati mwingine anafanya ujeuri mpaka anapotea apunguze utoto abadilike ili ndoto zake zitimie
Angelina
Akirud itakuwa vizuri
Zeiyana
Rose yupo vizuri sana majeraha aliyokua nayo ndio yanayo mfanya ashuke kwa kiwango chake alichokua nacho tunamatumaini hatakua na hujio mpya msimu huu
Neema juma
Arudi tu
David Pere
Kama bado kiwango anacho arudi tu maana Hali ni Tete pale anaweza kuisaidia
felister
you are welcome
Saupha mohamed
Arudi tuu
Sauda
Rudi kama panafaa
Lydia Emmanuel Magoti
Vizuri Kama anaitaji timu haludi tuu anamapenzi nayo Spurs
Isaya massawe
Dan rose mbona ni mchezaji mzuri tuu sema ndo hivo siyo chaguo la mourinho
Tatu
Itakuwa jambo zuri akiludi spurs danny rose
Ernest
Mourinho anatakiwa kumrudisha Rose kuokoa jahazi sio mchezaji mbaya
Furahav
Ongeza juudi urudi spurs.
Salma ngende
Angalia maslai yako
Gabriel
Habar njema
Issa
Rose kufanya hivyo ni sawa na kula matapishi yako
Mwanahamisi
Gud news
Rehema
Habari njema
Caroline
Aende tu spurs bado wanamuhitaji
Mwajumah
Arudi tu
warda
Ndo aombe tu Nafasi kipendacho roho #Meridianbettz
Sadick
Bado Mourinho ambaye hakumuhitaji yupo Tottenham, nadhani anatakiwa kufikiria kuendelea na mipango mingine nje ya Tottenham#meridianbettz
Devotha
Habari njema