Timu ya taifa ya Argentina imeendeleza rekodi yake ya kutopoteza nyumbani jijini Buenos Aires tangu ilipopoteza dhidi ya Uruguay Novemba 2023, baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Mauritania national football team katika uwanja wa Estadio Alberto J. Armando.
Argentina walianza mchezo kwa kasi kubwa, ambapo shuti la faulo la mapema la Julian Alvarez dakika ya nne lilimlazimisha kipa Babacar Diop kufanya kazi ya ziada kuokoa hatari. Hata hivyo, dakika ya 17 wenyeji walivunja ukimya kupitia kwa Enzo Fernandez aliyefunga kwa shuti la kwanza baada ya kupokea pasi safi kutoka kwa Nahuel Molina.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Bao la pili liliongezwa baada ya dakika 30, ambapo Nico Paz alipiga faulo maridadi kutoka nje ya eneo la hatari iliyomshinda kipa wa Mauritania. Licha ya ubabe wa Argentina, Mauritania walipata nafasi chache, huku jaribio la Oumar Ngom mwishoni mwa kipindi cha kwanza likimlazimisha kipa Emiliano Martinez kuokoa.
Kocha Lionel Scaloni alifanya mabadiliko kadhaa kipindi cha pili, akiwemo kuingia kwa Lionel Messi pamoja na Rodrigo De Paul na Franco Mastantuono. Hata hivyo, Mauritania walionekana kuwa na uhai zaidi, wakipata nafasi kupitia kwa Djeidi Gassama lakini alishindwa kulenga lango.
Licha ya kuwa na nyota wengi uwanjani, Argentina walishindwa kabisa kupiga shuti lililolenga lango katika kipindi cha pili, huku Mauritania wakiongeza presha. Dakika za mwisho, Jordan Lefort aliifungia timu yake bao la kufutia machozi na kufanya matokeo kuwa 2-1.
Baada ya mchezo huo, Argentina wanatarajiwa kucheza tena katika dimba hilo dhidi ya Zambia wakijiandaa kutetea taji lao la FIFA World Cup. Kwa upande wao Mauritania, licha ya kutofuzu michuano hiyo, wameonesha kiwango kizuri dhidi ya moja ya timu bora duniani.

