Mshambuliaji wa Sweden na klabu ya Arsenal, Viktor Gyokeres, amesema kuwa timu yake ina nafasi nzuri ya kufuzu Kombe la Dunia huku akibainisha kuwepo kwa hali nzuri ya morali kambini chini ya kocha mpya Graham Potter.
Sweden inajiandaa kucheza dhidi ya Ukraine katika nusu fainali ya mchujo wa kufuzu Kombe la Dunia itakayopigwa Valencia, Hispania.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Gyokeres ameweka wazi kuwa mabadiliko ya benchi la ufundi yameleta ari mpya kwa wachezaji baada ya kipindi kigumu kilichopita, ambapo Sweden ilishindwa kushinda hata mchezo mmoja katika mechi sita za hatua ya makundi.
Matokeo hayo mabaya yalipelekea kocha Jon Dahl Tomasson kuondolewa na nafasi yake kuchukuliwa na Potter kabla ya michezo miwili ya mwisho.
Kutokana na majeraha ya baadhi ya nyota wakiwemo Alexander Isak, jukumu kubwa la kuiongoza safu ya ushambuliaji limeangukia kwa Gyokeres. Hata hivyo, mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 27 amesema presha haimsumbui, akisisitiza kuwa anachoweka mbele ni kufanya kazi yake ipasavyo na kufunga mabao muhimu.
Ameeleza kuwa mchezo dhidi ya Ukraine utakuwa mgumu na wenye ushindani mkubwa, huku akitabiri kuwa nafasi za kufunga zinaweza kuwa chache kutokana na umuhimu wa mechi hiyo. Sweden inalenga kurejea kwenye michuano ya Kombe la Dunia baada ya kukosa fainali za FIFA World Cup Qatar 2022 miaka minne iliyopita.
Gyokeres pia amebainisha kuwa kuna mabadiliko makubwa ya kiufundi na kimazingira ndani ya kikosi hicho, jambo linalowasaidia wachezaji kusahau matokeo mabaya ya nyuma na kuelekeza nguvu kwenye malengo mapya. Ameongeza kuwa kikosi kina imani kubwa ya kufuzu na kiko tayari kupambana ili kufanikisha ndoto hiyo.
Katika hali ya kuvutia, beki Gustaf Lagerbielke amefichua kuwa baadhi ya wachezaji wamekuwa wakitumia muda wao wa mapumziko kujadili masuala mbalimbali ya maisha, ikiwemo nadharia za ajabu na mada za sayansi, jambo ambalo limeimarisha ukaribu na mshikamano ndani ya timu kuelekea mchezo huo muhimu.

