Yanga tayari imeshamtangaza mshambuliaji huyo ambapo ndio ulikuwa usajili wa kwanza kwa Yanga kutambulishwa msimu huu akitokea katika klabu ya Kaizer Chiefs ya nchini Afrika Kusini.
Kambole alisema kuwa anatamani kuona msimu ukianza mapema kutokana na hamu kubwa aliyonayo kuanza kuitumikia timu yake mpya ya Yanga ambapo matumaini makubwa kwake ni kuona anafanya vyema ndani ya Yanga.
“Natamani ligi ianze mapema hivi karibuni kutokana na kuwa na shauku ya kuanza kuitumikia Yanga katika michuano ya msimu ujao ya ligi na kimataifa ambayo tutashiriki.”
“Malengo yangu ni kuhakikisha kuwa nafanya vizuri zaidi nikiwa na Yanga kwa kuwa ni timu ambao imeonyesha kuwa inamalengo makubwa ya kufanya vizuri kwa msimu ujao na ndio maana nataka kuwa sehemu ya historia hiyo ya Yanga kwa msimu ujao,” alisema mchezaji huyo”
Kambole Autamani Msimu Mpya Bongo
Makala iliyopita
Feisal Apania Kufanya Makubwa Kimataifa
Makala ijayo
Nado Aanza Tizi Azam

