Thomas Frank Awatabiria Arsenal Kuwa Mabingwa

KOCHA wa Brentford Thomas Frank anaamini kuwa Arsenal ni washindani wa taji msimu huu, baada ya kutazama uchezaji wao wa kustaajabisha hadi sasa.

Kocha huyo aliona Arsenal wakiwa katika moja ya pointi zao za chini wakati timu yake ilipopandishwa daraja msimu uliopita, na kuambulia kichapo cha 2-0 kwa timu ya Mikel Arteta siku ya ufunguzi wa msimu huu.

Thomas Frank Awatabiria Arsenal Kuwa Mabingwa

Nice kickabout with the boys,” mshambuliaji wa Brentford Ivan Toney aliandika baada ya mechi ya kwanza kabisa ya msimu huu kwenye Ligi kuu.

Lakini rudisha nyuma fikra kwa zaidi ya mwaka mmoja Arsenal walikuwa nafasi gani, Frank anaamini Arteta amewabadilisha kabisa washika mtutu hao.

Thomas Frank Awatabiria Arsenal Kuwa Mabingwa

Arsenal walikaa kileleni mwa msimamo baada ya kushinda michezo mitano katika mechi sita za Ligi Kuu ya Uingereza, kabla ya Manchester City kuichapa Wolves mabao 3-0 na kuwapita siku ya Jumamosi mchana.

Hata hivyo, iwapo Arsenal watashinda siku leo dhidi ya Brentford, watarejea kileleni, na hapa ndipo Frank anatarajia wawepo mwishoni mwa msimu.

Thomas Frank Awatabiria Arsenal Kuwa Mabingwa

“Katika vipindi wamekuwa timu iliyofanya vyema katika mechi sita za kwanza,” Mdenmark huyo alisema.

“Nadhani zimekuwa za kushangaza, haswa nguvu. Nimetazama mechi zao nyingi, lakini mchezo wao wa kwanza, mchezo wa ufunguzi wa Ijumaa usiku dhidi ya Crystal Palace, nilikuwa nikifikiria nini? Hii ni hatua nyingine”.

 

Acha ujumbe