Trevoh Chalobah kumpisha Fofana.

 Trevoh Chalobah mchezaji wa klabu ya Chelsea ana uwezekano mkubwa kutolewa kwa mkopo kumpisha Wesley Fofana kutoka klabu ya Leicester City. Chelsea ipo mbioni kukamilisha dili la beki huyo wa kifaransa anaeitumikia klabu ya Leicester ya City.

Chelsea imepanga kumuachia beki huyo kijana waliompandisha kutoka shule yao kukuza vipaji maarufu kama Cobham kwa mkopo kuelekea klabu ya Red Bull Leipzig ya nchini ujerumani.

Chelsea wanapambana sokoni kuhakikisha timu inakua imara kwani mwalimu Thomas Tuchel anaonesha kutoridhishwa na sajili ambazo amezifanya kwenye majira haya ya joto kwani anahitaji watu bado kwenye kikosi ndo maana bado yupo sokoni kupambania saini ya beki ya Leicester City Wesley Fofana ambae atatoa nafasi kwa kijana Chalobah kutolewa kwa mkopo.

Chelsea kwa miaka ya karibuni wamekua wakiwatoa vijana wao kwa mkopo waliofuzu kwenye shule yao ya vijana ili wapate kupata uzoefu na kuja kuisadia timu hiyo mbeleni na Trevoh Chalobah anakua miongoni mwao.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.