Uefa Champions League Imerejea tena.

Uefa champions league imerejea tena na kuanza kutimua vumbi leo tarehe sita ya mwezi wa tisa mwaka 2022.

Pazia la ligi ya mabingwa barani ulaya ambalo linafunguliwa rasmi usiku wa leo na timu tofauti tofauti zitakua uwanjani kusaka alama tatu kwajili ya kujiwekeka mazingira mazuri kwenye msimu huu mpya wa ligi ya mabingwa ulaya.

uefa champions leagueMabingwa watetezi wa ulaya klabu ya Real Madrid itakua ugenini kuanza kampeni yake rasmi ya kutetea taji lao dhidi ya Celtic katika dimba la Celtic park.

Mchezo mwingine mkali utapigwa pale kwenye dimba la Parc de prince ambapo PSG watawakaribisha vibibi vizee vya Turin mchezo unaotarajiwa kua mkali sana kutokana na timu zote kua vizuri.

Michezo mingine mikali itakayopigwa leo ni kati ya Borussia dortmund vs Fc Copenhagen, Rb Leipzig vs vs Shakhtar donetsk, Dinamo Zagreb vs Chelsea, Sevilla vs Manchester City,Benfica vs Maccabi Haifa, Rb salzburg vs Ac milan.

 

Acha ujumbe